Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Niliitwa na Kuhojiwa Kuhusu Dawa za Kulevya na Wamebaini Sihusiki – Ridhiwani Kikwete

Mtoto wa Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema ameshahojiwa na kamisheni ya kupambana na Dawa za Kulevya na kukutwa hana hatia kuhusu tuhuma za kujihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya iliyokuwa ikimkabili.
Mbunge huyo wa Jimbo la Chalinze ambaye pia ni mwanasheria, jina lake lilitajwa kwenye list ya majina 97 ya watuhumiwa wa biashara haramu ya dawa za kulevya ambayo RC Makonda aliikabidhi kwa Kamishna wa kupambana na dawa za kulevya nchini, Rogers Sianga kwajili ya mahojiano.
Katika taarifa yake aliyoitoa Jumanne hii, Ridhiwani amesema ameshukuru kuona haki imetendeka katika sakata hilo lililokuwa likimkabili.
“Ni kweli niliitwa na kuhojiwa. Serikali yangu chini ya Kamisheni ya Madawa ya kulevya inasimamia haki na nimeona ikitendeka. Niko huru toka kwenye tuhuma/kashfa,” Ridhiwani aliandika Instagram.
Aliongeza, “Tuunge mkono juhudi hizi. Tuunge mkono hatua zinazochukuliwa ili kuokoa vijana wetu na kulinda nguvu kazi ya Taifa #vitadhidiyaMadawa #magufulinikazitu #tanzaniakwanza #miminikazitu #chalinzenikazitu,”
Alisema hiyo ni taarifa yake ya mwanzo kwa kuwa amebanwa na majukumu ya kazi na ukifika wakati atoa taarifa rasmi kuhusu sakata hilo.



This post first appeared on HABARI ZA SIASA NA MUZIKI, please read the originial post: here

Share the post

Niliitwa na Kuhojiwa Kuhusu Dawa za Kulevya na Wamebaini Sihusiki – Ridhiwani Kikwete

×

Subscribe to Habari Za Siasa Na Muziki

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×