Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

YOUTUBE VIDEO: JE UMEJENGWA KATIKA MSINGI YA MITUME NA MANABII WA MUNGU, AU UMEJENGWA KATIKA MISINGI YA MITUME NA MANABII WA UONGO?

YOUTUBE VIDEO: JE  UMEJENGWA KATIKA MSINGI YA MITUME NA MANABII WA MUNGU, AU UMEJENGWA KATIKA MISINGI YA MITUME NA MANABII WA  UONGO?
BABA katika jina la Yesu, ninawaombea wasikilizaji, ninawaombea watoto wako mahali popote ninawafungua kwa jina la YESU. MUNGU mkuu mwenye uweza  na mamlaka hakuna MUNGU kama  wewe, ninawatuma malaika wako pande zote, kila mahali kila nyumba, kwa kila kiumbe  kinachosikia ujumbe huu kwa jina la YESU ukaende kufanya mabadiliko kwa kila  mmoja katika jina la YESU wakapate kujua wewe ni MUNGU, wakazidi kusimama imara,  hata waliodondoka, waliokata tamaa, MUNGU wakakurejee au waliopotezwa katika jina la YESU, BABA ninakushukuru, Amen.
BWANA YESU asifiwe watoto wa MUNGU, katika kipindi cha leo nitaenda kufundisha kuhusu kujengwa katika misingi ya mitume na manabii wa MUNGU na kujengwa juu ya misingi ya mitume na manabii wa uongo. Nitasoma katika kitabu  cha Waefeso kile  cha pili mstari  wa ishirini  mpaka ule wa ishirini na mbili (Waefeso 2:20-22).

Neno la MUNGU linasema hivi; mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii naye Kristo YESU mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni. Katika yeye jengo lote linaunganishwa vyema na kukua hata liwe hekalu takatifu katika BWANA. Katika yeye ninyi nanyi mmejengwa pamoja kua maskani ya MUNGU katika Roho.
Bwana YESU asifiwe! katika somo hili la leo, Bwana YESU asifiwe ninakwenda kufundisha na kuvunja misingi mibovu. Misingi mibovu ni mafundisho ya shetani, haleluya….na misingi mizuri ya MUNGU ikapate kuingia ndani ya watoto wa MUNGU na MUNGU  akapate kutukuzwa na kufurahi, haleluya.. Kwa nini biblia inasema tumejengwa katika misingi ya mitume na manabii? Ndivyo ilivyo lakini misingi ya mitume na manabii tuliyojengwa nayo ni ile ya kweli, lakini sasa hivi mambo yamebadilika watu wamejengwa pia katika  misingi ya manabii na mitume wa uongo, vilevile nataka kukufundisha kwamba shetani alikopi kila kitu akabadilisha, utajiuliza kwa nini YESU alikuja  au  wakati anahubiri  akawa anapingwa, yeye alileta msingi wa kweli.

Lakini msingi wa uongo ulikua umeshaa tawala na YESU amekuja kutafuta kilichopotea, Bwana YESU asifiwe na kulijenga kanisa lake. Kama analijenga kanisa  lake nataka  uelewe vile vile na shetani analijenga la kwake lakini YESU anavyolijenga kanisa lake ni katika mafundisho ya neno la MUNGU la kweli sawa sawa na biblia ilivyo ambalo ndio msingi wa mitume na manabii wa kweli walioandika, wako kina  Musa, wako kina Eliya, Bwana YESU asifiwe wako kina Marko,wako kina Petro.

 Bwana  YESU asifiwe, walisema kweli ile ambayo ndio tunaifuata sasa hivi, kina Yeremia, lakini vile vile nataka nikujulishe mtoto  wa MUNGU, shetani na yeye ana Eliya wake wa kuzimu, ana Yusuph wake, ana Musa wake, ana Mathayo wake! Bwana YESU asifiwe, amekopi vile vile, na vimeletwa katika dunia hii sasa hivi watu wengi wamepotea, wanaona wapo katika msingi wa mitume na manabii wa kweli wa MUNGU lakini asilimia kubwa kwa kujua au kutokujua wako katika misingi ya mitume na manabii wa uongo, lakini nitakavyo kufundisha utakwenda kuelewa je wewe umejengwa katika msingi wa manabii na mitume wa kweli au umejengwa katika msingi wa mitume na manabiii wa uongo.
Bwana YESU asifiwe cha kwanza ukitaka kujua  wewe upo katika msingi  wa MUNGU wa kweli, tazama YESU alileta huduma  tano akasema Mtume na Nabii ndio kiongozi yeye hana askofu? Bwana YESU asifiwe, alileta Mtume na alileta Nabii, alileta Mwinjilisti, alileta Mwalimu, alileta Mchungaji, Bwana YESU asifiwe. Lakini sasa na shetani na yeye ana vya kwake hivyo hivyo Bwana YESU asifiwe, na mwanadamu unapokua unaongozwa au kusikiliza tayari na wewe unakua umejengwa  katika msingi wa mitume na manabii  wa uongo au wa kweli kivipi kupitia mafundisho ya uongo.

Ukisoma biblia, hii biblia takatifu imeandikwa na mitume na manabii wa kweli haleluya; tukaachiwa mafundisho ambayo YESU na yeye ni mmoja wapo wa mtume na nabii haleluya. Bwana  YESU asifiwe, hapo utakuta kuna ubatizo wa maji mengi  yanayotembea, unapoupata ule tayari na wewe unakua umejengwa  katika msingi wa mitume na manabii wa kweli ambao ni manabii na mitume wa MUNGU, lakini wewe ukiwa umebatizwa kinyume na ubatizo aliobatizwa YESU, haijalishi unasema kwa jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, wewe unakua kwenye ulimwengu wa roho na mwili tayari wewe umejengwa katika msingi wa manabii na mitume wa uongo kwa sababu huo ubatizo ni wa uongo sio wa kweli. Au unabatizwa kwa jina la mchungaji, kubatizwa kwa jina la mitume, hakuna  ni YESU peke yake ukiwa hivyo tayari wewe umejengwa katika msingi wa mitume na manabii wa uongo kwa hiyo huendi, nataka leo hiyo misingi ikavunjike na wewe umfuate YESU mahali ambapo unaona kuna YESU wa kweli alijenga misingi ya mitume na manabii wa kweli ndipo umfuate kinyume cha hapo umepotea.
YESU anarudi kuangalia kazi yake aliyoanzisha, je unafikiri atachukua msingi wa mitume na manbii wa uongo? unafikiri atachukua? Atachukua msingi alio uleta yeye kupitia manabii wake na mitume wake haleluya; maana MUNGU yeye niwa haki anaangalia neno lake, Bwana YESU asifiwe ukisoma Biblia YESU alileta wokovu lakini cha ajabu utakuta makanisa baadhi yanasema hakuna habari ya kuokoka, ninawaeleza huo ni msingi wa mitume na manabii wa uongo ambao hautaki wokovu, YESU alileta wokovu na bila kuwa na wokovu wewe hukamiliki kuwa mkristo, hakuna cha kukata shauri hakuna, ni  unatakiwa umekua mkristo umeokoka, wakatuletea kukata shauri, kataa, tafuta kwenye biblia hakuna jambo la kukata shauri ,ivi wewe unakata shauri? shauri ni nini? unatakiwa uokoke. YESU akija ataangalia msingi wake wa wokovu, je umeokoka? Lakini wengine wanakwua wamepotea wanasema mimi mlokole, mimi nakwambia YESU hajaleta msingi wa ulokole, hata kwenye biblia hakuna neno ulokole! Yeye alileta wokovu Bwana YESU asifiwe, kwa kingereza inaitwa salvation, sasa wewe umepokea ulokole au umepokea salvation?  

YESU ameleta wokovu, msingi wake, mnatakiwa muupokee, lakini vile vile unaweza kuta watu wameokoka, nataka niwaeleze kwa sababu mambo yamebadilishwa badilishwa sehemu nyingi hata katika mataifa  niliyotembelea.  Bwana YESU asifiwe! injili imebadilishwa na wana wa MUNGU hawaelewi wanampenda sana MUNGU lakini wengi wamejengwa katika msingi wa  manabii na mitume wa uongo! Asikuambie mtu kwamba yeye ametumwa na MUNGU  halafu hataki kubatizwa ubatizo wa maji yanayotembea  mtoni; huo sio msingi YESU aliouleta alisema mimi ndiye njia ya uzima na kweli nifuateni mimi nilivyofanya, aliingia mtoni Bwana YESU asifiwe akiwa mtu mzima sasa leo hii imebadilishwa uwe mtoto mdogo ndio unabatizwa tayari huo ni msingi wa mitume na manabii wa uongo, unajua mambo ya kiroho yamefichika sana lakini jinsi MUNGU anavyonipa neema  nakunfunulia nitakua nikiendelea kuwaelezea na zaidi endelea kusoma katika  website, katika blog; www.prophethebron.org utakuta mafundisho nikiendelea kuelezea na vitabu vingi mtajua ukweli, hata kama wewe umejengwa katika msingi wa manabii na mitume wa uongo utapona uchukue hatua, unaweza ukawa wokovu wako umejengwa katika misingi ya mitume na manabii  wa uongo.

Bwana YESU asifiwe, unabatizwa kwa jina la mchungaji wewe umejengwa katika msingi wa mtume na manabii wa uongo, umebatizwa kwenye kisima, hakuna huo ubatizo. Bwana YESU asifiwe, tafuta kwenye biblia ukisoma biblia inasema katika kitabu cha Ufunuo 22:18-19, ole wake aongezaye maneno ya  kitabu cha unabii  sehemu yake itaondolewa, ninakueleza ndivyo ilivyo na mafundisho yote ya uongo siyo msingi wa MUNGU. Bwana YESU asifiwe…Haleluya…MUNGU anawapenda sana ni wakati wa kuambiwa ukweli,YESU anarudi atakuja kuchukua alichokipanda yeye na kukivuna yeye, kama kimepandwa  na shetani au mpinga kristo utabaki huko huko, ukisoma biblia hii inasema msiabudu sanamu, ni ajabu wakristo wanaabudu sanamu  huo ni msingi wa mitume na manabii wa shetani, hayupo YESU hapo!
Jambo lingine endelea kusoma kitabu hiki Bwana YESU asifiwe, kuna watu wanafanya kazi ya MUNGU wanasubiri mshahara, na mwisho wa mwezi wanaenda kuchukua mshahara tena wanasubiri waongezewe. Bwana YESU asifiwe, na wanalipwa makato kama kawaida NCCF, PPF…Bwana YESU asifiwe, vitu ambavyo wanapewa watu wa kaisari; kwa MUNGU watumishi wake wanabarikiwa ila wale ambao wako upande ambao siyo wa MUNGU, wale wanaitwa watumishi wa mishahara ,na kama unaitwa mtumishi wa mishahara?
Wewe umejengwa katika msingi wa mitume na manbii wa uongo; ukibisha turudi katika neno hakuna mtumishi anatakiwa kupewa mshahara MUNGU kwa mtumishi anambariki soma neno hata kama unachukia; chukia lakini ukweli utabaki hapa hapa, tena mshukuru na mpone, maana yake shetani anakunyanyulia bango hata kama unampenda MUNGU, anasema huyu ni mtumishi wa mshahara….huyu ni mtumishi wa mshahara, je MUNGU una watumishi wa mshahara? neno lako linasema utawabariki kwa hiyo nataka muelewe  watoto wa MUNGU watumishi wa MUNGU hawana mshahara wanabarikiwa basi!
Sasa siku hizi wamenyanyuka wakutafuta pesa au wa misingi ya shetani; wakujiita, misingi ya mitume na manabii wa uongo. MUNGU yeye anamuita mtumishi wake, anapomuita anampa chanel na direction ya kazi yake haleluyaa..habahatishi lakini misingi ya mitume na manabii wa uongo, mtu atakwambia nimeongea na MUNGU, sawa! Ameongea na mungu shetani pia ni aina ya mungu, ataanzisha huduma zitaitwa kwa jina la YESU, zina upako  wake, zina uponyaji wake, lakini ukija ukiangalia misingi ya mitume na manabii huku, nimekupa bure toa bure, wewe utasikia leta pesa yako ndio MUNGU atakufungua, ninakwambia huo ni msingi wa mitume na manbii wa uongo hauwapeleki mbinguni mtaangamia rejeeni kwa MUNGU acheni hayo mambo, na wako watu wengi hata wokovu wao haukui, hata hawabadiliki  kwa sababu umejengwa chini ya misingi  ya mabii na mitume wa uongo, japo wewe muumini haujui, hayo ninakufunulia ukapate kuelewa…haleluya...

Watu wengi wanaomba sana wanasoma biblia, umejengwa kwenye msingi wa uongo wewe, unakuja unasema….nasimama na kitabu fulani neno litakua hili, haliwi! kwa nini? jiulize kwanza  msingi wako wewe asili yake jichunguze, umejengwa katika misingi ya  mitume na manabii wa kweli au  wa uongo, kivipi utajuaje? Angalia mafundisho ya uongo au mafundisho ya kweli. Bwana YESU asifiwe, au kanisani kwenu mnatoa huduma kwa kuchaji pesa  Bwana YESU asifiwe, maana na shetani ana miujiza yake…haleluya…
Katika misingi ya mitume na manabii wa uongo  kazi zao za injili ni lazima wachangishe pesa, YESU alivokuja alivyoingia hekaluni alikuta wanafanya biashara, alifukuza maana siyo mahali pake kwahiyo makanisa ukikutaa  mahali wanachangisha pesa wa elfu laki moja simama hapa huo ni msingi  wa mitume na manabii wa uongo na ukikaa hapo na baraka zako zimejengwa katika hao, mfilisi,masikini na Mbinguni huendi. Ninachokwambia ndicho hicho lakini katika msingi wa mitume na manabii wa MUNGU, aliojenga kwa ajili ya kanisa lake linalopeleka watu Mbinguni linakujenga wewe, katika nyumba yake hakuna harambee nawaeleza mkichukia mchukie!

Tusome kwenye biblia hakuna mahali imeruhusiwa kufanyika kanisani. Kama kazi ni ya kwake mtumishi arudi kwa MUNGU amuulize yeye, kama amejengwa kwa misingi ya mitume na manabii wa kweli wa MUNGU, amrudie yeye ataona njia zinafunguka,lakini waliojengwa katika misingi ya mitume na manabii wa uongo  watarudi hapo hapo,na wengine hata walianza  na MUNGU  lakini  wamepotea kwa sababu ya kufuata hayo mambo ya elimu za uongo za wanadamu.
Mtu atakwambia ni Doctor  pamoja na degree yake lakini ukiangalia anafanya vitu kinyume na MUNGU. MUNGU haangalii hicho kazi hiyo inafanywa na Roho Mtakatifu, inawezekana hata upo darasa la tatu  MUNGU akakutumia, unajua kusoma biblia tu basi…haleluya...Roho mtakatifu mwalimu wa kweli anaingia ndani. Bwana YESU asifiwe. 

Hayo ni mambo umekua ukisikia. Sasa hivi huduma watu ni wachawi, watu ni washirikina, Mchungaji ni mshirikina, mara anatoa watu kafara, nini hiyo nachowaambia ni misingi ya mitume na manabii wa uongo,mara mwingine atakwambia anadondosha watu angani nakwambia hivi, msingi wa mitume na manabii wa MUNGU  wa kweli wanaonyesha watu kinachofufuliwa kama wanabisha wapelekee hapo maiti  watakimbia! Lakini wanataka watengeneze njia njia za kudondosha dondosha watu kataeni hii misingi na hata kama mnashiriki unajenga ufalme wa misingi ya  mashetani pasipo wewe kujua  lakini wewe ukifikiri kwamba unamjengea MUNGU.

Hatakama unaimba hapo unapoabudu ujue kwamba kwenye ulimwengu wa roho inabadilishwa wewe hapo unamwimbia mungu wa manabii wa uongo ambaye ni lusifa, joka kuu na serikali yake wanatukuzwa na mpinga kristo, ni ajabu sana Bwana YESU anarudi alipokuwa akiniambia mambo haya nilikua naogopa sana maana nilikua mtoto mdogo sana kama miaka minne hivi kiroho, Bwana YESU asifiwe, nakutuma kwa mataifa yote misingi imeharibika imebaki asilimia mbili( 2%) , hata sasa nimeanza kwenda na bado nitazunguka dunia nzima, na yeye ndiye atanipeleka kwa jina la YESU njia zake MUNGU ni MUNGU na zitafanyika tu.
Nahakikisha misingi hii iwaachilie wana wa MUNGU, watasikia sauti ya MUNGU watabadilika siyo kwamba watakuja wote, wa shetani wapo. Bwana YESU asifiwe, kwa nini neno la MUNGU linasema acheni magugu na ngano yakue pamoja, mengine yatabadilika yatakua ngano ila yakikataa yabaki kua magugu, yawezekana wewe ni ngano lakini ukikaa na magugu ukikataa kubadilika nawe utakua hivyo hivyo, inamaana kwamba  ukikaa na msingi mbovu nawe unakuharibu Bwana YESU asifiwe…haleluya..msiogope watoto wa MUNGU, YESU anarudi, ili wewe utengenezwe wewe akukute na akuchukue kubali kujengwa katika kweli ya neno lake…haleluya…
Cha kwanza hakikisha umetimiza ahadi zote;  umeokoka,umebatizwa, hutendi dhambi, unaisha maisha ya kitakatifu, YESU hayo ndiyo aliyoyaleta, wanadamu mwogopeni MUNGU, msimuone MUNGU ni rafiki au jirani. MUNGU hafananishwi na kitu, msimuone MUNGU niwakuchezewa. BwanaYESU asifiwe, ametulia, wakati wake unakuja, watu watalia na kusaga meno, huu ni wakati wa neema ninawaeleza watoto wa MUNGU, mahali popote ulipo mrejee Bwana YESU, uliyejengwa katika msingi wa uongo hutaki kuokoka acha, na ndio maana kuna watu hawataki kuokoka  kabisa hata ukiokoka wanakwambia umechanganyikiwa, yeye amejengwa katika msingi wa mitume na manabii wa uongo ambao ile roho imekaa ndani yao kwa hiyo anashangaa wokovu ni nini lakini unakuta anang’ang’ania YESU, wewe siyo rafiki wa YESU umegombana na YESU, kubali leo upatane na YESU, hii dunia itapita mambo yatapita haleluya..hao marafiki wataishia kaburini.
Bwana YESU asifiwe, utakapoingia kaburini ule mwili wako ndio utapambana na yeye, huko hakuna wa kukusaidia, hakuna wa kuongea na wewe, wakati wako ni sasa Bwana YESU asifiwe…haleluya..nitatoa labda mfano mwingine ili muelewe, Bwana YESU asifiwe, kuna neno linaitwa kafiri! Bwana YESU asifiwe, maana ya kafiri ni mtu yeyote ambaye haendi sawa sawa na neno la MUNGU lilivyo, kwa hiyo unaweza kukuta mtu anasema kafiri, lakini yeye mwenyewe ajichunguze kwanza ndani yake je anafuata sheria za MUNGU? ameokoka? anasema kweli? anahubiri kweli? au ananyang’anya watu pesa? Sasa akiwa kinyume hivyo yeye ankua ni kafiri. Bwana YESU asifiwe, je unafikiri YESU atakuja kuchukua kafiri? 

YESU anakuja kuchukua mtu ambaye siyo kafiri, Bwana YESU asifiwe, nataka nielezee maana hii ya kafiri ni mtu yeyote ambaye hafuati sheria za mwenyezi MUNGU,ni mtu ambaye yeyote hamfurahishi MUNGU, siyo umchekee kutoa meno bali kubali sheria zake na amri zake, sasa hapa duniani tayari umekua kafiri au umekua siyo kafiri ni wewe mwenyewe uamue, unataka kuwa kafiri au kwenye maisha ya kafiri au unakuja kwa YESU? Mimi nakwambia njoo kwa YESU, usiwe kafiri  Bwana YESU asifiwe, lakini makafiri nataka uelewe hapo,wapo makafiri wakubwa wa kiroho ambao ni watumishi, na wako makafiri wadogo, hao makafiri wakubwa ndio hao watumishi ambao wanatumia  uongo,na kutumia neno la MUNGU katika uchawi, utawajuaje hao makafiri? Kwa matendo yao, neno la MUNGU linasema hivi….kwa mtumishi wangu niliyekujenga katika msingi wa mitume na manabii wa kweli, nimekutuma wewe usifikiri utapata pesa wapi, mimi nitakuongoza utapata pesa njia zitafunguka haleluya..lakini wanao ongozwa na kafiri hao manabii na mitume wa uongo katika ulimwengu wa roho katika ufalme wa shetani, watakaa kwenye TV, na kuomba pesa na M-PESA kumwaibisha mwenyezi MUNGU, MUNGU wetu siyo masikini, MUNGU wetu ana kila kitu, kazi zaoni kunyang’anya watu, watu mpaka wamechoka, hawataki habari za MUNGU zimewakwaza mimi nawaambia hivi. Zilizo wa kwaza siyo za MUNGU, siyo za YESU habari za YESU wa kweli na MUNGU wa kweli kama umekutana naye zina neema, zinafurahisha, zinakuponya wewe funguka sasa mrejee MUNGU wa kweli…haleluya..usiogope anakupenda, wako malaika wanakuangalia ni wakati wa kuharibu ufalme wa ma shetani, lakini hautaitwa wa shetani maana kuna makanisa ndiyo ya shetani, lakini shetani ana mbinu nyingi amekopi biblia!
YESU alianzisha kanisa akasema na ubatizo wa maji mengi, naye akaanzisha wa maji kidogo, haupo mbinguni huo, unasema unakwenda mbinguni, mbingu ipi utakwenda? wanakwambia  hivi ukisoma katika msingi wa mitume na manabii wa kweli, MUNGU wetu si MUNGU wa wafu, huu mwingine wanatengeneza kwamba ukifa tutakuombea, ninakwambia toka mwaka 1949, hakuna rais aliyeingia au mfalme mbinguni paradise. Kama ni watu wanaombewa ni hao, MUNGU anaangalia haki haangalii cheo chako Bwana YESU asifiwe, anakuangalia kama alivyokuleta umekaa katika line yake? kama hujakaa katika line come now! this is your time. Bwana YESU asifiwe, hakuna mambo ya kuogopa,unayeogopa mimi nakuombea  usiogope, walipokushika na kukushindilia MUNGU anakwenda kukunyanyua, misingi iliyokujenga naenda kuivunja, ikuachilie maisha yako, ikuachilie ukaokoke, ikuachilie ukapate kutawala na kumiliki,ukatembee kama mwana wa MUNGU kifua mbele.
Sasa hivi watu wengi wameokoka yaani ndiyo wana shida,wana shida, shida si ya kwao wamejengwa katika misingi ya manabii wengi wa uongo, ni viliyo, hakuna watu wanalia shida kama wakristo, mimi nakwambia asilimia kubwa omba omba, lile jina unapolipata  la huyu YESU anasema mtakua nuru kwa nini hamuwi nuru? Umasikini ndio umejaa, shida zimejaa,wakristo wachawi, haiwezekani Bwana YESU asifiwe,  yeye MUNGU awafungue macho,YESU anarudi, ulikuja mwenyewe mwanadamu sijui utarudije. Amenituma kwako nikueleze, mimi amenituma habari njema ndio hizi nakwambia, habari mbaya sasa hivi ni nyingi zinasambazwa, injili za uongo za uongo za uongo maana shetani anatajirishwa na watu wake nataka uelewe! Bwana YESU asifiwe, ni wakati wa kumsimamisha 

Bwana YESU..haleluya..hili jina la YESU linatumika vibaya kwa sababu wanadamu wanajua ya kwamba  jina hili linapendwa na shetani naye amelichukua analitumia vile vile kwa watumishi wake, nataka nikwambie kuna watumishi wanaenda kuzimu kabisa, anapewa uchungaji na shetani, uinjilisti, unabii anasema naye na ndio maana utashangaa kuna mtu anasema unabii alafu inakua ni muongo, sasa huyo mungu ni muongo, ndio msingi wa manabii wa uongo.
Bwana YESU asifiwe, kama nilivyokwisha kuwaambia Tanzania ndio taifa linaenda kunyanyuka na limeshaanyanyuka dunia nzima itakuja kusarenda hapa, MUNGU ameniambia na ndivyo ilivyo, msingi wa nabii na mitume wa kweli na neno lake linatimia,walio wa kwanza watakua wa mwisho, na wa mwisho watakua wa kwanza, nchi iko mikononi mwake nilikwisha kusema hakuna uchawi hapa nchi itabadilika hata wanao iba iba pesa miaka minne watu walioona napiga kelele mmeyaona sasa na bado YESU yupo kazini anawatu wengi atawatumia hao hao, Bwana YESU asifiwe msiogope, imefika mahali nchi hii haiendi vizuri, wachawi tu laity ungekua na macho, wengi ni wachawi wanakaa makanisani lakini wanaenda kuzimu wanapanda na kushuka wanapanda na kushuka kuharibu  hata uchumi kuharibu viongozi, kuharibu bunge wasielewane, kuna wakati utashangaa hata wabunge wanatukana tukana tu, Bunge haliombewi; tuliombee. Bwana YESU asifiwe ni wanadamu pale ni vita bana pale wakikaa vizuri nchi itaenda vizuri!
Wasameheane hata yaliyotokea Bwana YESU asifiwe, mipango yote ya wachawi haitafanikiwa ni mpango wa Bwana YESU dini nyingine wanamwita nabii Issa, kila mahali inajulikana anayekuja nabii wa mwisho kuchukua kanisa kuchukua watoto wa MUNGU ni nabii Issa, wewe umemkubali Bwana YESU? mkubali sasa kama hujajengwa chini ya msingi wake leo na sasahivi  ndio nafasi yako wa kweli usikubali kujengwa katika msingi wa YESU wa uongo, hakuna wokovu ni michango, Bwana YESU asifiwe, hata ukitaka kubatizwa unatoa ada, unajua hata serikali ni nzuri sana haichaji kanisa kodi, inahofu na MUNGU, Bwana YESU asifiwe ,lakini huku wako baadhi yao wanafanya mambo yao kwa kuharibu jina la Bwana YESU, simama umtetee Bwana YESU, msingi wa mitume na manabii wa kweli, ukisoma Biblia anasema hivi, MUNGU anasema hivi, usilipe riba,usichaji riba, lakini leo hii unakuta makanisa ya mitume na manabii yana benki yanachaji riba, nataka uelewe hao wamejengwa juu ya misingi ya mitume na manabii wa uongo na waumini ni huko huko wanakwenda kwa muongo, baba yao atakua ni muongo, maana MUNGU analiangalia neno lake. 

Kuna mbinu nyingi sana anaweza akakwambia kwamba ameongea na MUNGU amefika mpaka anapelekwa kuzimu anaongea na shetani, si baba yake hawezi muita shetani nataka uelewe…haleluya...Bwana YESU asifiwe, mnasikia watoto wa MUNGU? lakini jeuri yao imekwisha, njia zao zimekwisha kufungwa…haleluya...YESU atanyanyuliwa na ni wakati wake wa YESU wa kweli sasa kusimama ndio…vita vitaendelea lakini YESU atashinda tu! Na nakwambia wewe ambaye unashindwa kila siku nitakuombea utashinda utasonga mbele..haleluya…zaidi karibu katika kanisa la YESU NI BWANA NA MOKOZI WA MATAIFA YOTE nitakuombea na mambo mengine utaendelea kufunguliwa.
Bwana YESU asifiwe, ingia katika website yangu www.prophethebro.org ingia katika link ya blog na youtube Bwana YESU asifiwe, karibu sana na utafunguliwa kuna vitabu, Bwana YESU asifiwe nataka mumuelewe MUNGU, mimi nilikua si mtu wa kuhubiri, nilivyokutana na YESU kwanza nilikua namshangaa akili yangu mimi nilikua nimejengwa katika msingi wa mitume na manabii wa uongo kwa hiyo sura ya YESU nikajua ni yule mwingereza Brian, hizi picha mnasema ni YESU. YESU anakuja anaongea na mimi ninamkemea, ninamkemea, ninamkemea, nilikuja kutubu baadaye baada ya kunielewesha, wala hafanani wala hakuna sura ya Bwana YESU hapa yeye ni MUNGU hata jicho lake huwezi kuchora, Bwana YESU asifiwe,uku wake na uweza wake niwa ajabu, hapa duniani mnaona ona kuna vitu, hakuna vitu!
Mbinguni nimefika yako makao yanakusubiri wewe, kuzimu pia nimekwenda nikaoneshwa na YESU palivyo, siyo huyu YESU mnayeoneshwa picha za Brian hapa, hizi anaact huyo siyo YESU. Nimefika mbinguni nimepaona ,nimepelekwa kuzimu nimepaona na kuzimu inavyokushangilia inakusubiri wewe, Bwana YESU asifiwe, nimewakuta wachungaji, maaskofu, mitume, manabii wengi wako huko ambao duniani walikua wanajulikana ni watumishi haswa kumbe ni mapepo tu! Na hata waliopo hapa duniani mnaona wanaendesha kazi zao kichawi chawi, wako kule kuzimu kwa hiyo wanakua connected na shetani kuintroduce kazi zao huku na branch zao zinasambaa, wewe unapokaa tuu pale nafsi yako imeshavunwa YESU hakupati, nataka sasa ukapate kusimama.
Misingi ya mitume na manabii unakuta eti mchungaji anjiita MUNGU, soma biblia ni nani anayefananishwa na MUNGU? hakuna ! mrejee Bwana YESU …haleluya...mtatolewa na ishara za uongo na shetani anaweza hivyo hivyo, kumbukeni kipindi cha Musa, farao naye akatengenezewa nyoka, zaidi njoo kwenye neno la MUNGU hatua kwa hatua, muulize wewe unasema ni mkristo je mbona hujabatizwa kama YESU? Tuchambue ubatizo gani uliwekwa na YESU? wa misingi ya uongo siko huko! Toka rejea uokoke ukabatizwe upya usimame imara, usiimbe hapa wewe ni mkristo unaenda mbinguni kila siku jumapili, kumbe unaenda kukonektiwa kupigiliwa misumari kila wiki  unaenda kuwa msingi mbovu kataa! Bwana YESU asifiwe.Ukisoma katika misingi ya mitume na manabii wa MUNGU, tumepewa roho mtakatifu atuombee, tafuta hakuna mahali ipo Petro anatakiwa atuombee! Hakuna mahali iko Musa, hakuna mahali iko jina la Frank hakuna la mtu yoyote nakazalika,mtume yeyote hapa, hakuna! tunaye ruhusiwa kumuomba yuko Roho mtakatifu, ni mambo yameharibika watoto wa MUNGU na leo watu wamejengwa katika misingi hiyo, hiyo misingi ya mitume na manabii ya uongo, nawe umekua ni muongo, mkristo muongo mbele za MUNGU wala MUNGU hakutambui, iko neema MUNGU amenituma kwako wewe rejea, haleluya Bwana YESU asifiwe.

Nilikua mahali fulani, nikashangaa sana,ukisoma misingi ya mitume na manbii waliojengwa na MUNGU, nimekupa bure toa bure, mtumishi kwenda kumuona anakwambia dollar mia kumsalimia, hao niwaongo, kusikilizwa pesa waongo, unapewa na risiti hao ni waizi! Na wewe ukristo wako hujajengwa na MUNGU, umejengwa na shetani, lakini hujui ni shetani wanasema shinwa shindwa shetani, shindwa shetani,hakuna ufalme ambao unaweza ukaharibu ufalme mwingine, kataa ondoka huko, Bwana YESU asifiwe, mrejee Bwana YESU wengi wamepotezwa, wengi wanalia,wengi wamekata tamaa, Bwana YESU asifiwe. Nimekuta kuna mafuta ya upako, unajua MUNGU wa mbinguni siyo mlanguzi, unakuta mafuta yanauzwa elfu tano au elfu sita dukani mchungaji mwingine anauza laki mbili! Je wananchi au wanadamu wana moyo wa ukarimu zaidi kuliko MUNGU? sasa huku kutafuta vitu wizi! Lakini ni maagano ya kishetani, MUNGU awafungue macho wewe unayesikiliza, Bwana YESU asifiwe, utaenda kwenye semina, kwenye maombi sana lakini unakutana na mapepo, nakueleza kama ulikua hujui, sasa ukaelewe Bwana YESU asifiwe. Lakini nakutia moyo neema yake ipo bado, anarudi YESU angalia usikutwe umejengwa kwenye misingi ya mitume na manabii wa uongo.

Kanisa mtu Baba yake na watoto wake ndio wanalichukua hayaa! Umeangalia vitu kama hivyo,watu wanafanya makanisa ni sehemu ya kupata pesa si mahali pa kumwabudu mwenyezi MUNGU, ni mahali pa kwenda kukaa na amani, we umeenda kutafuta amani kabla hujaondoka simama mchango wa kwaya kama kwaya ni ya MUNGU hiyo sadaka unayotoa wakati wa sadaka si inafanya kazi hiyo? haya kikapu cha Mama mchungaji ni msingi wa uongo!Bwana YESU asifiwe, sijui mchungaji anasimama unamsainia hela  nisainie kwenye shati! ni misingi ya manabii wa uongo, au unakuta kanisani,wanakujua  kiasi chako unaitwa Gold wewe saizi ya Gold , Almasi lulu, wanaangalia pesa yako huyo ni msingi wa  manbii wa mitune wa uongo  wa shetani hata unaitwa umedanganywa unaliwa pesa wala MUNGU hajapokea zimepotea na unazidi kuvuna umasikini unajenga ufalme shetani na unaingia katika hukumu hiyo, uliwekwa hapa duniani ukafanye kazi ya MUNGU, ukaende kufanya kazi ya MUNGU na kuombea hata kumsifu ili siku moja  kule mbinguni ukavalishwe taji, tazama siku ile ya mwisho,utavalishwa taji na shetani kama ulikua hujui elewa sasa, amenituma kwako elewa  kwa mataifa yote. 

Bwana YESU asifiwe...msiogope, Bwana YESU asifiwe, MUNGU anawapenda watu wake wote, wala yeye habagui, tatizo ni ukafiri umeingia, ukafiri sasa wewe unasema unamfuata MUNGU, jichunguze matendo yako kama hauko sawa na MUNGU, neno linaitwa kafiri halikuachi na mimi sitaki muwe kafiri, Bwana YESU asifiwe, kile kilichokua kafiri nataka kibadilike kimrejee Bwana MUNGU.
Bwana YESU asifiwe ili siku moja urudi na wewe Mbinguni, lakini na hapa duniani umfurahie MUNGU. Bwana YESUasifiwe haleluya..Bwana YESU asifiwe, msiogope watoto wa MUNGU, MUNGU anawapenda sana, alipokuwa akinieleza mambo haya mpaka natoa machozi Bwana YESU alikua akinieleza Mbinguni yupo na Petro aliyekua mwanafunzi wake  hata wao kina Yeremia walioandika biblia wako mbinguni na kina Daudi na kina Yohana na muda wa kurudi YESUumeshafika,wameshamaliza maandalizi  yote mpaka ya hukumu, na mimi sasa ninakufunulia siri hii nabii wake MUNGU, rejea kwake hukumu isikukute  tazama utasema nasubiri lini utabadilika mpaka kesho au lini  usimwambie MUNGU ukampangia time,time yako na sasa hujui yajayo kesho. MUNGUhana mpango na watu ambao hawamtaki sasa hivi,wanasema wakati mwingine tutakua tuna time na MUNGU inamaana unavyosema hivyo inamaana una time na shetani, sasa sema time ya shetani sitaki bye bye.
Bwana YESU asifiwe, yawezekana hata hujaokoka lakini wewe ni mkristo kumbe uko katika msingi mbovu ondoka sasa simama imara  biblia inasema tokeni  mkatengwe nao ukakae mahali ambapo kuna neno la kweli lisiloghoshiwa, utaambiwa neno lisiloghoshiwa lakini watu wanabatizwa kwa kisima na neno lisiloghoshiwa  hapo utasikia watu wanaandika majina  wanapewa risiti hii imekua biashara. MUNGU haangalii pesa zako, Bwana YESU asifiwe, siku moja nilikua naongea na mtu mmoja  hii misingi ya aibu, moja mtumishi mmoja wa mahali fulani ana kanisa sasa viatu vyake vimetoboka akaingia madhabahuni siku ya ibada akaanza kunena rikoboshondo rakashika akaanza kulia anajifanya anaomba MUNGU, ananena…  baba wasamehe kanisa hili…wamemuacha mchungaji wao mpaka viatu vimetoboka... wasamehe baba usiwapige, kanisa zima likaanza kulia saa hiyo hiyo wakaenda knunua viatu… wakamletea mchungaji madhabahuni akavalishwa, eti wanaomba rehema!huyu ni muongoo…MUNGU watumishi wake hawajiabishi yeye hana shida. YESU anarudi na katika ulimwengu wa roho wachawi wanajua, kuzimu wanajua na wako wanadamu ambao ni watumishi wa shetani na wao wanajua….anarudi yuko njia, dalili zimeshatimia, mambo yao hayaendi. YESUanakwenda kunyanyuliwa, toka kwenye mgome ya mashetani.
Sema BWANA YESU, NINAOMBA UNISAMEHE DHAMBI ZANGU ZOTE NILIZOZIFANYA KWA KUJUA AU KUTOKUJUA. UKANIVUNJIE MISINGI YOTE MIBOVU NDANI YANGU ILIYOJENGWA NA MITUME NA MANABII WA UONGO. IKABAKI MISINGI YA MITUME NA MANABII WA KWELI ULIYOIJENGA WEWE BWANA YESU, UNIONGOZE NA JINA LANGU ULIANDIKE KATIKA KITABU CHAKO CHA UZIMA. AMEN
NABII HEBRON. 


This post first appeared on UNABII WA KWELI, please read the originial post: here

Share the post

YOUTUBE VIDEO: JE UMEJENGWA KATIKA MSINGI YA MITUME NA MANABII WA MUNGU, AU UMEJENGWA KATIKA MISINGI YA MITUME NA MANABII WA UONGO?

×

Subscribe to Unabii Wa Kweli

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×