Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Dk. Hamisi Kigwangalla Apanga Mkakati Wa Kujenga Makumbusho ya Marais Wastaafu

Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii inatarajia kujenga makumbusho ya Marais Wastaafu wa Tanzania.


Hayo yameelezwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla wakati akizungumza na Balozi wa Uingereza hapa nchini, Sarah Cooke ofisini kwake mjini Dodoma.

Dk. Kigwangalla amemueleza balozi Cooke kuwa, Serikali kupitia Wizara yake inaendelea kuimarisha vivutio vya utalii hapa nchini kwa kupanua jeografia ya maeneo ya utalii sambamba na kuongeza vivutio ili kuongeza idadi ya watalii na mapato.

Amesema Serikali itajenga makumbusho ya Marais Wastaafu wa Tanzania mjini Dodoma pamoja kuanzisha makumbusho ya meno ya tembo katika miji ya Dar es Salaam, Arusha, Iringa na Dodoma.

Sambamba na hayo amesema Serikali itaanzisha mwezi maalum wa maadhimisho ya urithi wa Mtanzania ambao utafanyika mwezi Septemba kila mwaka pamoja na kuendeleza utalii wa mikutano.

Amesema Serikali pia itaanzisha Mamlaka ya Usimamizi na Uendelezaji wa Fukwe nchini ili kuimarisha utalii wa fukwe pamoja na kutambua barabara iliyokuwa ikitumika katika biashara ya utumwa wakati wa ukoloni ili iweze kutumika kiutalii.


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Dk. Hamisi Kigwangalla Apanga Mkakati Wa Kujenga Makumbusho ya Marais Wastaafu

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×