Young Africans (Yanga) inarudiana na Welayta Dicha ya Ethiopia mjini Sodo, lakini ikiwa na faida ya magoli 2-0 iliyopata kwenye Mechi ya awali. Mchezo huo utaonyeshwa Azam Sport Two saa kumi kamili jioni
Timu zingine Kutoka Afrika Mashariki ni Gor Mahia ya Kenya na Rayon Sport ya Rwanda zitashuka dimbani leo kwa ajili ya mechi za marudiano za hatua ya mtoano katika kombe la shirikisho barani Afrika.
Gor Mahia itakuwa mjini Pretoria nchini Afrika Kusini kucheza na wenyeji wao Supersport United, na ili kusonga mbele mabingwa hao wa Kenya itawalazimu kulinda ushindi wa goli 1-0 waliopata katika mechi ya kwanza.
Mabingwa wa Rwanda Rayon Sport, wao watakuwa nchini Msumbiji kurudiana na Costa Do Sol ambayo katika mechi ya awali wakiwa mjini Kigali waliifunga timu hiyo magoli 3-0.
Endapo timu hizo zitapa ushindi wa jumla baada ya mechi hizo, moja kwa moja zitafuzu na kujumishwa katika mechi za hatua ya makundi.
Droo ya kupanga mechi za hatua ya makundi itafanyika jumamosi ijayo Aprili 21 mjini Cairo.