Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Maofisa 28 wa JWTZ Wapandishwa Vyeo na Rais Magufuli



RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli ameridhia na kuwapandisha vyeo Maofisa 28 wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kuanzia jana Aprili 12, 2018 huku akimbadilisha Msaidizi wake Kanali Mbaraka Mkeremy ambaye amempandisha cheo na atapangiwa kazi nyingine jeshini.

Aidha, Rais pia amekukubali kumpandisha cheo kutoka Luteni Kanali kuwa kanali D.P.M Murunga na kuwa mpambe wa Rais akichukua nafasi ya Kanali Mkeremy.

Akitoa taarifa ya uteuzi huo, Mkuu wa Majeshi, Jenelari Venancy Mabeyo amesema maofisa walioteuliwa wanakwenda kuimarisha safu za utendaji kazi kijeshi na kwamba maofisa wote hao watavalishwa vyeo vyao Ijumaa hii katika makamo makuu ya Jeshi Upanga Jijini Dar es salaam.

Katika uteuzi huo Rais Magufuli amewapandisha vyeo maofisa wa ngazi mbalimbali Jeshini ikiwa ni pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma Kanali M E Gaguti ambaye sasa anapanda cheo na kuwa Brigedia Jenelari na kurejeshwa Jeshini.


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Maofisa 28 wa JWTZ Wapandishwa Vyeo na Rais Magufuli

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×