Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Taarifa za Awali Zatolewa Juu Ya Uchunguzi wa Kupigwa Kwa Risasi Mpalestina Mmoja


Msemaji wa Jeshi la Israel tarehe 10 ametoa taarifa akitangaza matokeo ya awali ya uchunguzi kuhusu mdunguzi kumpiga Risasi Mpalestina, na kukitaja kitendo hicho kuwa "mbinu ya mwisho baada ya kushindwa kuwatawanya wapelstina kwa njia zisizo za kuwaua".

Juzi video kuhusu mdunguaji wa jeshi la Israel kumfyatulia risasi mpalestina ilisambaa kwenye mtandao wa Internet, ikionyesha mdunguaji mmoja akimfyatulia risasi mpalestina aliyekuwa karibu na uzio wa mpaka kati ya Israel na Gaza, , na askari wa jeshi la Israel waliokuwepo walionekana kushangilia baada ya kuona mpalestina huyo akianguka kutokana na kujeruhiwa na risasi.

Msemaji wa jeshi la Israel amesema video hiyo ilipigwa mwezi Desemba mwaka jana kwenye ukanda wa Gaza. Askari hao kwenye video wataadhibiwa, na jeshi la Israel litachunguza tukio hilo kwa pande zote.

RFI


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Taarifa za Awali Zatolewa Juu Ya Uchunguzi wa Kupigwa Kwa Risasi Mpalestina Mmoja

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×