Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Klabu Bingwa Ulaya (UEFA): Mechi za Marudiano za Hatua ya Robo Fainali Kupigwa Leo na Kesho


Mechi za Robo Fainali ya klabu bingwa barani Ulaya zinarejea leo kwa michezo miwili ya marudiano itakayopigwa kwenye miji ya Manchester na Roma.

Nchini Uingereza, Manchester City watakuwa katika uwanja wao wa nyumbani kuwaalika wainegeza wenzao Liverpool.

Katika mechi hiyo ambayo inatabiriwa kuwa ngumu kwao, Man City wanatakiwa kushinda magoli 4-0 ili kusonga mbela bila kikwazo, baada ya wao kukubali kipigo cha magoli 3-0 kwenye mechi ya kwanza iliyopigwa mjini Liverpool.

Lakini nchini Italia AS Roma watakuwa nyumbani kuwa kawakaribisha Barcelona kutoka Hispania ambao tayari wana mtaji wa kusonga mbele kutokana na ushindi waliopata kwenye mchezo wa kwanza wiki iliyopita wa magoli 4-1.

Mbali na mechi za leo, hatua hiyo ya robo fainali itaendelea kesho kwa mechi mbili pia, Bayern Munich dhidi ya Sevilla na Real Madrid dhidi ya Juventus.

Washindi wa jumla wanne kutokana na mechi hizo, watafuzu nusu fainali na droo ya kupanga mechi za nusu fainali itafanyika ijumaa hii April 13.


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Klabu Bingwa Ulaya (UEFA): Mechi za Marudiano za Hatua ya Robo Fainali Kupigwa Leo na Kesho

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×