Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAONESHA UBABE MASHINDANO YA RIADHA SHIMIWI



Na. Mwandishi Wetu, Iringa

Wizara ya Maliasili na  Utalii imeendelea kuonesha ubabe wake kwenye mbio
ambapo kwa upande wa wanaume imeibuka kinara  kwenye mbio za mita 1500 na  mshindi wa pili kwenye mbio za mita 400 huku  kwa upande wa wanawake  imeibuka   mshindi wa tatu kwenye mbio za mita 1500 katika Mashindano ya 37 ya Shirikisho la Michezo la Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) yanayoendelea Mkoani Iringa .

Akizungumza leo mkoani humo mara baada ya ushindi huo Bw. Elibariki Buko ambaye ndiye mshindi wa mbio namba moja wa mita 1500 na namba  mbili za mita 400,  amesema ushindi huo ni matokeo ya  uongozi makini wa Menejimenti ya  Wizara ya Maliasili na Utalii

" Ushindi huu  sio wa kwangu mimi  bali ni ushindi wa Wajumbe wa Menejimenti ya Wizara ya Maliasili na Utalii, wamekuwa msaada mkubwa  kwetu kuanzia maandalizi hadi hatua hii. Niwashukuru sana Mimi pamoja na watumishi wenzangu kwa  kuendelea kutuwezesha kushiriki katika  michezo hii.

Ametumia fursa hiyo  kuihakikishia Menejimenti ya Wizara hiyo kuwa yeye pamoja na wenzake watatumia michezo hiyo kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini huku akiomba kuendelea kupewa nafasi zaidi katika kushiriki katika mashindano mengine  ili waweze kukidhi ndoto na maono aliyonayo Rais Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan kwenye sekta ya utalii kitaifa na kimataifa.


, ‘’Tumeanza kutangaza utalii na vivutio vya utalii vilivyopo maeneo haya kama Hifadhi ya  Ruaha na hata vivutio vingine kama Hifadhi ya Taifa ya Nyerere." amesema Buko.

Ameongeza,’’ imetusaidia pia  kujenga ushirikiano na afya kwani  nina uhakika mara tukaporudi katika maeneo yetu ya kazi umakini na uhodari katika kuhudumia watanzania utaongezeka’’ 

Kwa upande wake Jehovaness Sarakikye ambaye ndio mshindi wa tatu kwenye mbio za mita 1500 kwa wanawake amesema, aliamini atashinda mbio hizo mara baada ya kufanya maandalizi ya kutosha huku akiwapongeza Walimu kwa kuwaandaa vzuri kwa ajili na shindano huo

‘’Tulijiandaa vizuri, haikuwa rahisi lakini nawashukuru sana Walimu wetu walifanya kazi nzuri ya kutuandaa kwa ajili mchezo huu’’ Alisema Sarakikye

Naye Mratibu wa Timu ya Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Leodger Kiwia   ametumia fursa hiyo kuwapongeza washindi hao kwa kuipatia ushindi Wizara huku akisisitiza kuwa Wizara itahakikisha inaendelea kupambana ili kushinda michezo iliyobakia na hatimaye kubeba vikombe vyote.

" Nawapongeza sana Washiriki wetu wote ikiwemo na hawa wa Riadha, ushindani ulikua mkali sana lakini hatimaye wameiletea Wizara yetu furaha. Sisi kama Viongozi tutaendelea kusaidia wachezaji hawa kwa namna yeyote ile ili watuletee ushindi na hatimaye tupeleke vikombe nyumbani’’ Amesema Kiwia



This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAONESHA UBABE MASHINDANO YA RIADHA SHIMIWI

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×