Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

TASAC WASHIRIKI KATIKA MAONYESHO YA BIASHARA YA SABASABA



AFISA Masoko Mwandamizi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Martha Kelvin akitoa elimu kwa mmoja wa wananchi waliofika kwenye Banda lao katika Maonyesho ya Sabasaba yanayoendelea Jijini Dar es Salaam

 Mwananchi aliyetembelea Banda la TASAC akipatiwa zawadi katika Banda la TASAC

Watumishi \wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Martha Kelvin wa pili kutoka kushoto akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wengine wa Shirika hilo wakiwa kwenye Banda lao



Na Mwandishi Wetu,Dar es Saalam

Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania, TASAC linashiriki katika maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa.

Maonesho hayo yenye Kauli Mbiu “Tanzania Mahali Sahihi Pa Biashara na Uwekezaji”, yameanza tarehe 28 Juni, katika viwanja vya Sabasaba Jijini Dar es Salaam na yatahitimishwa tarehe 13 Julai , 2023.

Akizungumza leo Afisa Masoko Mwandamizi wa Shirika hilo Martha Kelvin alisema lengo la kushiriki maonesho hayo ni kujenga uelewa na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu kazi na majukumu yanaotekelezwa na TASAC kwa mujibu wa Sheria ya Uwakala wa Meli Tanzania, Sura 415 na mabadiliko yake.

Hata hivyo alisema kwamba TASAC inawaalika wananchi wote kutembelea maonesho haya na kufika katika banda la TASAC lililopo katika ukumbi wa Karume banda namba 22 na 23.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

TASAC WASHIRIKI KATIKA MAONYESHO YA BIASHARA YA SABASABA

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×