Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

LORI LAUA WAENDESHA BODABODA ZAIDI YA 10 KIJIWENI

Tags: eneo tukio hilo

Watu kadhaa wamepoteza maisha baada ya lori lililokuwa likisafirisha changarawe kupoteza mwelekeo na kugonga kundi la bodaboda waliokuwa wameegesha Eneo lao (kijiweni) mjini Migori nchini Kenya.

Tukio Hilo la asubuhi ya Jumamosi - Aprili 8,2023 limeshuhudia umati mkubwa wa watu ukimiminika eneo la Tukio ili kuwanusuru majeruhi na kuwakimbiza hospitalini kwa matibabu. 

Kwa mujibu wa raia mmoja aliyeshuhudia na kuzungumza na runinga ya TV47, breki za lori hilo zilifeli na kuingia katika kundi hilo la bodaboda ambao walikuwa wanasubiri abiria. 

Ajali hiyo imefanyika karibu na shule ya msingi ya Migori. Eneo la tukio lilikuwa limejaa damu na miili. 

Vyuma pia vilikuwa vimetapakaa eneo hilo.

Eneo la tukio linaripotiwa kuwa na zaidi ya miili kumi huku ambulansi na wazima moto kutoka kwa serikali ya kaunti ya Migori wakifika eneo la ajali hiyo.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

LORI LAUA WAENDESHA BODABODA ZAIDI YA 10 KIJIWENI

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×