Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

MCHUNGAJI ALIYEBAKA NA KUWAPA MIMBA BINTI ZAKE ATUPWA JELA MIAKA 140...ASEMA ALIPITIWA NA SHETANI



Mahakama nchini Kenya imemfunga Kifungo Cha Miaka 140 jela mchungaji aliyewabaka wasichana wake wawili wa miaka 14 na miaka 16 na kuwapatia mimba.

Akitoa hukumu hiyo hakimu mkazi wa Baricho Anthony Mwicigi, alimuhukumumwanaume huyo kifungo cha miaka 70 kwa kila msichana . Mahakama iliamua kuwa hukumu hizo zitatekelezwa moja baada ya nyingine na hivyo mchungaji huyo ataishi jela miaka 140.

Mchungaji huyo kutoka kaunti ya Kirinyaga kati kati mwa Kenya, mwenye umri wa miaka 51 alikiri Kuwabaka Watoto Wake tarehe 5 Januari na kuwekwa jela tangu tarehe 7 Januari. Alimlaumu shetani kwa ubakaji huo watoto wake na akawaomba msamaha watoto wake na mahakama.

Hakimu mkazi Anthony Mwicigi alisema kuwa mchungaji huyo alipataikana na hatia kwa kukiri mwenyewe kuwabaka watoto wake na akaagiza hukumu dhidi yake itolewe tarehe 14 Januari.

Mchungaji huyo anayefahamika kwa jina la Gichina alikamatwa mahala alipokuwa amejificha baada ya polisi kuanzisha harakati za kumsaka.


Msichana mmoja tayari ana mtoto wa miezi 7 na mwingine ana mtoto wa miezi 5.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

MCHUNGAJI ALIYEBAKA NA KUWAPA MIMBA BINTI ZAKE ATUPWA JELA MIAKA 140...ASEMA ALIPITIWA NA SHETANI

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×