Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

DED KYERWA AWATAKA VIJANA KUWA WABUNIFU,KUTAMBUA VIPAJI VYAO



Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kyerwa Shedrak Mohamed

Vijana wilayani Kyerwa mkoani Kagera wametakiwa kuwa wabunifu katika  masuala mbali mbali ya  kiuchumi kuliko kusubiri ajira kutoka serikalini.

Kauli hiyo imetolewa leo Agosti 13,2019,na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kyerwa Shedrak Mohamed katika mwendelezo wa wiki ya uwekezaji Kagera yenye lengo la kutangaza fursa za mkoa wa Kagera.

Mohamed amesema vijana wanatakiwa kubuni na kutambua vipaji walivyonavyo kuliko kukaa bila kazi huku baadhi wakisubiri ajira kutoka serikalini.

Mkurugenzi huyo amesema kuwa katika wilaya yake ya Kyerwa kipaumbele ni kwa vijana ili kujenga taifa imara na lenye nguvu.

Amesema vijana wanatakiwa kuchangamkia  fursa mbalimbali za mikopo zinazotolewa na halmashauri.

Hata hivyo ametoa wito kwa jamii kufanya kazi bila kubagua ili kujikombia kiuchumi kutokana na mkoa wa Kagera kuwa na fursa mbalimbali.
Na Lydia Lugakila - Malunde1 blog Kagera










This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

DED KYERWA AWATAKA VIJANA KUWA WABUNIFU,KUTAMBUA VIPAJI VYAO

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×