Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

POLISI WATOA AMRI YA KUKAMATWA KWA MKE WA RAISI MSTAAFU NI BAADA YA KUMPIGA MWANAMITINDO


Polisi nchini Afrika Kusini imetoa amri ya kukamatwa kwa Grace Mugabe, mke wa aliyekuwa rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ambaye anatuhumiwa kumshambulia na kumjeruhi mwanamitindo wa Afrika Kusini, Gabriella Engels, mwaka 2017.

Mwanasheria anayefanya kazi na shirika la kutetea haki za binadamu la AfriForum la huko Afrika Kusini, Garrie Nel amesema amethibitishiwa na Polisi kuhusu kutolewa kwa amri hiyo, na kuongeza kuwa ikiwa Bi. Mugabe atakanyaga kwenye ardhi ya Afrika Kusini atakamatwa.

Mwanasheria huyo vile vile ametaka mchakato wa kumtia mbaroni Grace Mugabe na kumsafirisha hadi Afrika Kusini uanze sasa.

Grace Mugabe anatuhumiwa kumpiga na kumjeruhi mwanamitindo Gabriella Engels kwenye hotel moja mjini Johannesburg Agosti mwaka 2017, lakini hakushtakiwa kwa sababu alikuwa na kinga ya kidiplomasia.
chanzo:Eatv


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

POLISI WATOA AMRI YA KUKAMATWA KWA MKE WA RAISI MSTAAFU NI BAADA YA KUMPIGA MWANAMITINDO

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×