Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Mo Dewji kuificha Simba mikononi mwa Juventus ya Italia


Mohammed Dewji amepanga kuiunganisha Simba kwa Juventus ya Italia. Tajiri huyo namba moja kwa sasa hapa nchini alitua Italia katika klabu hiyo mapema wiki hii na kufanya nao mazungumzo juu ya kuinua soka la Tanzania. Akiongea na mtandao wa Salehjembe, Dewji amesema, “Wiki hii nilifanya kikao na Juventus FC. Wanayo nia ya kuendeleza soka kwa vijana wa Tanzania. Ninatazamia kuitambulisha timu hiyo ya Italia kwa uongozi wa Simba SC ili waanze majadiliano ya jambo hilo.” Juventus imekuwa ikishirikiana na baadhi ya nchi za Afrika katika kuendeleza mchezo huo ikiwemo Libya (wakati ikiwa tulivu), Tunisia, Morocco na Misri.


This post first appeared on HABARI ZA SIASA NA MUZIKI, please read the originial post: here

Share the post

Mo Dewji kuificha Simba mikononi mwa Juventus ya Italia

×

Subscribe to Habari Za Siasa Na Muziki

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×