Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Napigania kuachia albamu mwaka huu, ikishindikana nitauzia dukani kwangu - Cyrill Kamikaze

Rapper Cyrill Kamikaze amefunguka juu ya mpango wake wa kuachia albamu kama walivyofanya Navy Kenzo na baadhi ya wasanii walioahidi kufanya hivyo Mwaka huu.
Akiongea katika kipindi cha Flavour Express cha Maisha FM, Silver Touchez, Rapper huyo amesema anapigania kuachia albamu mwaka huu japo kwenye swala la uuzaji ndio tatizo lakini ikishindikana atauzia hata dukani kwake.
“Mimi nini ngoma nyingi sana zipo studio. Actually nina ngoma nyingi mpaka nyingine zimekuwa outdated kwa sababu nimekuwa nikirekodi sana. Situation ya kutoa albamu Bongo imekuwa tatizo kidogo nikisema nitoe nitajuliza nitaanzia wapi kuiuza?,” amesema Cyrill.
“Lakini kuanzia mwaka jana, mwaka juzi ilikuwa ni ndoto yangu lakini kunakuwa na mambo mengi yanaingiliana. Lakini mwaka huu ninataka kupigania hili suala niwe na albamu mkononi na ikishindikana basi nitaiuza hata dukani kwangu,” ameongeza.



This post first appeared on HABARI ZA SIASA NA MUZIKI, please read the originial post: here

Share the post

Napigania kuachia albamu mwaka huu, ikishindikana nitauzia dukani kwangu - Cyrill Kamikaze

×

Subscribe to Habari Za Siasa Na Muziki

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×