Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

YAJUE MAGONJWA YANAYOATHIRI FIGO


Figo ni kiungo muhimu kwa ajili ya kuchuja vitu mbalimbali ikiwamo sumu kwenye Damu, mkojo na maji yasiyohitajika ili kuwa na kiwango kinachohitajika cha maji na madini (electrolytes) mwilini.

Licha ya hayo, hufyonza madini na kemikali muhimu kuzirudisha katika mzunguko wa damu huku ikitoa nje uchafu usiohitajika.

Kutokana na umuhimu wake, inashauriwa kuchukua hatua zote makini ili kuepusha maambukizi yanayoweza kuathiri uwezo wa kiungo hiki kufanyakazi kama inavyotakiwa.  Magonjwa mengi yanayoweza kuathiri figo husababishwa na mfumo wa maisha kama vile unywaji wa pombe na uvutaji sigara.

Mfumo wa maisha ambao husababisha magonjwa yasiyoambukiza kama vile kisukari yanaongeza hatari ya magonjwa ya figo au kama unavyotambulika Chronic Kidney Disease (CKD).

Kushambuliwa kwa figo kunaweza kusababisha ikashindwa kabisa kuendelea kufanyakazi, inapofikia katika hatua hii tiba sahihi huwa ni dialysis au kuchuja maji yasiyohitajika mwilini na uchafu unaambatana na maji hayo.

Tiba hii hutolewa kwa wale ambao aidha figo zao zimeshindwa kufanya kazi au wana upungufu wa figo moja ambayo huelemewa.  Upo uwezekano wa mgonjwa kupandikizwa figo nyingine kutoka kwa mchangiaji.

Matibabu haya yote hugharimu muda, fedha na rasilimali nyingine za mgonjwa hivyo kuna umuhimu wa kujiepusha na mazingira hatarishi kwa kadri inavyowezekana.

Miongoni mwa mambo muhimu ambayo yanashauriwa ni kuepuka magonjwa yasiyoambukiza ambayo athari zake zina uwezekano mkubwa wa kufika kwenye kiungo hiki na kukipotezea uelekeo wake.  Yapo magonjwa ambayo unapaswa kuyaepuka.

Kisukari

Kisukari ni moja ya magonjwa yanayoongoza kuleta athari Kwenye Figo kwa kuharibu mirija inayopeleka damu, na inayofyonza damu kutoka kwenye figo na kusababisha ishindwe kusafisha damu kwa usahihi.

Matokeo ya changamoto ni mwili kuwa na kiasi kikubwa cha maji na chumvi kuliko inavyohitajika, hivyo kusababisha kuwapo kwa taka nyingi mwilini.

Madhara mengine ni mkojo kushindwa kwenda kwenye kibofu, kutokana na kuharibika mrija unaousafirisha kutoka kwenye figo kwenda kwenye kibofu au urethra.

Kutokana na hili mkojo hulazimika kurudi kwenye figo na kuziweka kwenye hatari kutokana na msukumo mkubwa unaokuwapo, wakati mwingine kutokea maambukizi ya njia ya mkojo.

Shinikizo la Juu la Damu

Shinikizo la damu ni ugonjwa unaotokana na kuwapo kwa msukumo mkubwa wa damu kuliko kawaida.  Ongezeko la msukumo huu kwenye mishipa ya damu husababishwa na mapigo ya moyo kwenda kupita kiasi.

Msukumo wa damu mwilini unapokuwa mkubwa sana, unaweza kusababisha mishipa ya damu hasa iliyopo kwenye figo kukaza, kuitengenezea majeraha madogo na kutokana na msuguano unaotokana na msukumo mkubwa wa damu uliopita; kuidhoofisha na kukosa nguvu.

Kutokana na hali hii basi, mishipa ya damu iliyopo kwenye figo inaweza kuisababisha ishindwe kuchuja uchafu kama inavyotakiwa.  Pia, vimiminika vinavyosalia ndani ya mishipa ya damu baada ya figo kushindwa kufanya kazi kwa usahihi, vinaweza kuongeza shinikizo la juu la damu na hatari zake.

Kukabiliana na shinikizo inashauriwa kula vyakula ambavyo havina kiwango kikubwa cha mafuta, kufanya mazoezi ya viungo na kuzuia msongo wa mawazo.

Lehemu

Lehemu au cholesterol ikizidi mwilini huleta shida.  Kuzidi kwa mafuta haya kunatokana na ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi hasa ya wanyama na kutofanya mazoezi.

Lehemu ikizidi mwilini, inaenda kujijenga ndani ya mishipa ya damu ambayo inasafirisha damu kutoka na kuingia kwenye figo hivyo kuathiri utendaji kazi wake.

Uwepo huu wa lehemu katika mishipa ya damu inaweza pia ikasababisha shinikizo la juu la damu na kisukari.  Vipimo vya damu vinaweza kuonesha kama kiwango chako cha lehemu kipo juu ama la.

Matatizo wakati wa haja ndogo (urine blockage)

Kama unashindwa kupata haja ndogo au unaipata kwa shida inaweza kumaanisha mkojo unarudi kwenye figo kabla ya kufika kwenye kibofu na inaweza kuleta madhara kwenye kibofu.

Kutokana na uwapo wa mkojo ambao unashindwa kutoka nje unaongeza uwezekano wa kupata maambukizi kwenye figo na sehemu nyingine za mwili.  Tezi dume lililoongezeka ukubwa, saratani ya tezi dume, uwepo wa mawe katika figo, saratani ya kibofu, damu kuganda katika njia ya mkojo na saratani ya utumbo ni baadhi ya magonjwa yanayosababisha tatizo hili.

Ni vyema kumuona daktari haraka au kama unaona mchanganyiko wa damu unapokojoa.

Lupus

Mwili una mfumo kinga maalumu wa kujilinda na kujikinga dhidi ya magonjwa mbalimbali kuingia mwilini kwa kutumia kinga zake unaojulikana pia kama immune system ukiwa na jukumu la kushambulia viini vyote vya magonjwa vinavyoingia mwilini.

Wakati mwingine mfumo huu hukosea na kushambulia tishu mbalimbali za mwili na kusababisha ugonjwa wa lupus.  Dalili zake viungo vya mwili kuuma, homa za mara kwa mara, maumivu ya kifua, kunyonyoka kwa nywele, vidonda vya mdomo na kuhisi kuchoka mara kwa mara.

Kinga za mwili zinaposhambulia tishu za mwili huweza kufika mpaka kwenye figo na kusaabisha ugonjwa unaoitwa lupus nephritis ambao huchangia kutokea kwa michubuko kwenye mirija inafyonza maji kutoka mwilini hatimaye kuzifanya figo kushindwa kufanya kazi ipasavyo.


Mazoezi ya mara kwa mara na kufanya vipimo vya kitaalamu ni mambo yanayoshauriwa kwa watu wote na muda wote.  Hii ni bila kujali umri wa mhusika.


This post first appeared on Afya Na Kiasi, please read the originial post: here

Share the post

YAJUE MAGONJWA YANAYOATHIRI FIGO

×

Subscribe to Afya Na Kiasi

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×