Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

TANZIA: Video Queen Maarufu Nchini Agness Masogange Afariki Dunia




Msanii anayepamba video za muziki (video queen), Agnes Gerald ‘Masogange’ amefariki dunia leo.

Taarifa hizo zimethibitishwa na mwanasheria wake, Reuben Simwanza

Simwanza amesema taarifa za Kifo Chake amezipata kupitia Dada Yake, saa chache zilizopita.

Kwa maelezo ya Simwanza, dada wa Masogange, Emma Gerald, ndiye aliyetoa taarifa hizo baada tu ya kutoka kumuona alipokuwa amelazwa katika Hospitali ya Mama Ngoma, Mwenge jijini Dar es Salaam.

Mwanasheria Huyo Ambaye amedai yeye si msemaji zaidi, kuhusu nini chanzo cha kifo chake, alidai mara ya mwisho waliwasiliana naye siku mbili zilizopita kwa ujumbe wa simu ya mkononi.

 “Unajua kuumwa kweli alikuwa anaumwa, kipindi cha kesi yake magonjwa ya hapa na pale ikiwamo presha, si unajua tena mambo ya kesi hayana mwenyewe, lakini baada ya kwisha tulikuwa tunataniana kwamba sasa nina imani utakuwa powa kwani kila kitu kipo sawa,”amesema Simwanza.

Hata hivyo amesema yupo njiani kuelekea hospitali kwa kuwa hakuweza kupata maelezo zaidi kutoka kwa dada yake huyo ambaye amemsikia akiwa analia tu.


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

TANZIA: Video Queen Maarufu Nchini Agness Masogange Afariki Dunia

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×