HD kirefu chake ni High Definition - ni picha yenye ubora zaid ya SD kirefu chake ni Standard Definition kama kwa mfano unavyoonekana hapo chini!
Ili uangalie katika mfumo wa HD ni lazima kama ni tv iwe ni HD pia na utumie cable maalum inayoitwa HDMI CABLEHD imegawanyika katika ubora tofauti kutokana na Technology kuendelea kukua kila kukicha
- HD - 720p ( 1280x720 )
- Full HD - 1080p ( 1920x1080 )
- ULTRA HD 4K- 2160p ( 3840x2160 )
- ULTRA HD 8K- 4320p ( 7680x4320 )
Ukiwa una tv HD unapaswa pia uwe na vishiriki HD navyo, mfano uwe na King'amuzi ama Ving'amuzi DH na DVD pia iwe HD dhumuni la kukushauri utumie vishiriki HD navyo ili uweze kuona picha katika muonekano wa HD, kwanini!? ikiwa tv ni HD ukitumia king'amuzi ama DVD ambayo sio HD hautaona picha katika mfumo wa HD na hata kama utatumia king'amuzi ama DVD HD lakini ukatumia cable ya AV hautaona picha katika mfumo wa HD badala yake utaona picha katika mfumo wa SD ili uone katika mfumo wa HD ni lazima utumie cable ya HDMI CABLE
Ukiachilia hilo kuna baadhi ya picha zenyewe zipo katika mfumo wa HD na ndicho ambacho kinafanywa na wadau wengi wa mambo ya film Productions iwe kwenye vituo vya matangazo ama watengenezaji wa filamu..
Kwa Tanzania tunatumia sana HD na Full HD lakini kwenye Ultra HD nisiwe muongo bado sijakutana nazo ama aliyekutana nazo aniambia hapa..