Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

KUEPUKA DISH YAKO KUPATA KUTU

Niwe mkweli katika hili usipopata fundi makini uwezekano wa kuepuka hili ni mdogo sana vinginevyo muhusika uwe makini sana na Fundi wako ingawaje mara nyingi muhusika inakuwia vigumu kuona jinsi fundi wako alivyofunga Dish huko juu ya paa!!

Sababu zinazopelekea Dish kupata kutu kwa haraka:-

Sababu zisizoepukika:-

> Ikiwa Dish inafungwa ufukweni.

> Ikiwa Dish ni FAKE.

Sababu zinazoepukika:-

> Kutokuweka vinavyozuia maji kuingia.


Tuone madhara ya kutotumia vinavyozuia maji kuingia ndani na kukosa pa kutokea!
1
Hii ni Stendi ya kubeba Dish,hiki ni kikalio ( Chini ) ambapo kwa kutokufunika juu,imesababisha Maji yameingia na kwakuwa hakuna sehemu maalumu ya kutokea maji yanapoingia,yenyewe yakatafuta njia kwa kutafuna kidogo kidogo mpaka kupata njia kama muonavyo!

2
Huu ni mkono wa kushika LNB,upo mfano wa V,mkono huu ni bomba maana yake kati lipo wazi,upande wa mbele inafungwa LNB ambapo inazima maji kuingia na upande wa nyuma kuna ya kukipachika Ili Kuzuia Maji yasiingie kama ilivyoonyeshwa picha namba ( 5 ) kwakuwa yakiingia kinachotokea pale kwenye mkunjo ndipo maji yatajitengenezea njia kama muonavyo hapo juu!
3
Matokeo yake ile V inageuka vipande viwili baada ya kuliwa na kutu!
4
Ufungwaji Dish wa namna hii ndio unaopelekea madhara tuliyoyaona hapo juu kwenye picha ( 1 - 3 ) jinsi maji yalivyosababisha kutu,ambapo kama fundi angetumia vifaa vyote ipasavyo yasingetokea madhara hayo yaliyotokea!
5
Hivi ndivyo unavyopaswa kufunga Dish yako kwa kutumia Plastic cover ili kuzuia maji yasiingia kwenye bomba ya Stend na mkono wa kushika LNB!

Nadhani kwa uchache umeambulia kidogo kwa maelezo zaidi
+255789476655 
NB:Kupiga kuanzia saa 08:30 - 18:00 


This post first appeared on Mustapha MaDish Tech, please read the originial post: here

Share the post

KUEPUKA DISH YAKO KUPATA KUTU

×

Subscribe to Mustapha Madish Tech

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×