Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Obama na Putin wajadiliana kuhusu Ukraine


Rais Obama amefanya mazungumzo zaidi ya kina na rais wa Urusi Vladmir Putin akisistiza kuwa vitendo vya nchi yake Katika jimbo la Crimea ni ukiukaji wa mipaka na uhuru wa taifa la Ukraine.
Wakati wa mazungumzo yao ya pili kupitia njia ya simu katika Kipindi Cha Siku sita zilizopita, bwana Obama amependekeza njia ya kusuluhisha mzozo huo kidiplomasia inayojumuisha Urusi kuwaondoa wanajeshi wake katika jimbo la Crimea. Bwana Putin amesema uhusiano kati ya Moscow na Washington haufai kutatizika kutokana na mzozo wa Ukraine.
Awali bwana alisema kuwa kura ya maoni iliyopendekezwa kuhusu jimbo la Crimea kujiunga na Moscow inakiuka sheria ya kimataifa na sharti ijumuishe serikali ya Kiev iwapo itaandaliwa.
Akizungumza baada ya mkutano mwingine wa Baraza la Usalama uliofanyika faraghani, balozi wa Uingireza katika umoja wa mataifa , Mark Lyall Grant, amesema haiwezekani muafaka kupatikana katika baraza hilo kuhusu mzozo huo.
"Nadhani hakuna dalili kwamba kutakuwa na mwafaka katika baraza la usalama Katika Kipindi Cha Siku Chache Zijazo. Kama ulivyosikia kutoka kwa wengine, kuna mashauri yanayoendelea kati ya wanadiplomasia kwenye mikutano mbali mbali Ulaya. Mashauri hayo yataendelea,'' amesema bwana Grant.
''Pengine kiwango fulani cha makubaliano kitaafikiwa ili kutuliza mgogoro huu na kisha baraza la usalama pengine litapata suluhu. Lakini hatujafutilia mbali mpango wa kuwasilisha azimio mbele ya Baraza la Usalama wakati wowote na tunafuatilia hali ya mambo kwa karibu tukitarajia baraza la Usalama likutane tena katika siku chache zijazo ikitegemea kitakachotokea mashinani."
Mzozo huo wa Ukraine umechochea wanasiasa pamoja na wageni wengine mashuhuri kususia mashindano ya Olimpiki ya wanariadha walemavu nchini Urusi. Marekani imeondoa ujumbe wake katika michezo hiyo na mawaziri wa Uingereza hawatakuwepo sawia na wenzao kutoka mataifa mengine ya Ulaya.
Habari na BBC SWAHILI


This post first appeared on Mchambuzi@habari Online, please read the originial post: here

Share the post

Obama na Putin wajadiliana kuhusu Ukraine

×

Subscribe to Mchambuzi@habari Online

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×