Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

JE UNAJUA KAMA HUJABATIZWA KWA UBATIZO WA MAJI MENGI WEWE SIYO MKRISTO KABISA! SOMA HAPA UJUE UKWELI

Tags: sasa yesu agano
JE UNAJUA KAMA HUJABATIZWA KWA UBATIZO WA MAJI MENGI WEWE SIYO MKRISTO KABISA! SOMA HAPA UJUE UKWELI
Nawasalimu kwa jina la Yesu WA NAZARETI aliye hai na ndiye aliye mwana wa pekee wa MUNGU Sasa na milele, wala hatakuwepo mwingine zaidi yake. YESU huyu yeye ndiye agano la MUNGU kati yake na wanadamu ili kwa kupitia yeye watu wafike mbinguni na wamuone MUNGU na zaidi hata biblia inamtaja kuwa yeye ndiye njia ya uzima na kweli. Sasa niwaulize swali watu waote wa mataifa, je ipo njia nyingine tena ya kweli ya kutupeleka mbinguni ambayo MUNGU ameleta tuifuate? Jibu, haipo. Ni YESU WA NAZARETI peke yake au kwa jina lingine anaitwa Nabii Issa.
Nitaelezea kwa ufupi kuhusu mkristo anayejiita yeye ni mkristo lakini hajabatizwa kwa maji mengi yanayotembea. Nilipokuwa nafundishwa na YESU mimi Hebron, sikuyajua haya na mengi sana ila ilibidi anifundishe yeye mwenyewe kwanza kabla ya kunituma kuifanya kazi yake sababu sikusomea katika chuo chochote hapa duniani ila mwalimu wangu ni yeye YESU WA NAZARETI. Alinifundisha kama alivyowafundisha wale wanafunzi wake wa kwanza. Akaniambia watu wanapigwa upofu na shetani ili wasije mbinguni wala wasinione nao wengi wao wananipenda ila hawapo katika njia ya kweli, wapo katika njia ya mwovu ambayo ni ya shetani. Wametekwa na mafundisho ya uongo nao wamekuwa watoto wa baba wa uongo ambaye ndiye Ibilisi. Sasa nakutuma Henron uwaeleze mataifa yote ukweli na watakao yatii maneno niliyokutuma watapona ila watakao yakataa damu yao haitamlilia MUNGU katika mikono yake. Katika biblia hakuna ubatizo wa maji ya kikombe, wala maji ya kisima, wala mtu kubatizwa kwa jina la mchungaji yeyote yule. Batizo za jinsi hii zote ni batizo za agano la kuwa wewe ni mfuasi wa shetani, ila wewe haujui ni siri iliyofichika. Amenituma YESU, sasa muelewe na mwatumie na wengine ujumbe huu na zaidi soma kitabu cha UBATIZO WA KWELI KWA ULIMWENGU WOTE cha Nabii Hebron utaelewa zaidi.
Ili uwe mkristo ni lazima uokoke na ubatizwe kwa ubatizo wa maji mengi tena ukiwa mtu mzima, unazo akili. Nataka muelewe hata siku zote mtu unapoingia mkataba wowote hapa ulimwenguni ni lazima uusome, uuelewe, ndipo uukubali, usaini. Sasa nikuulize swali ulipokuwa mtoto mdogo ulielewa kuwa unabatizwa? Na ulikuwa unayo akili? Na je neno ubatizo ni kumwagiwa maji kichwani tu? Jibu, siyo. Kubatizwa ni kuzamishwa. Sasa uone tu hapa tayari haujabatizwa ila umemwagiwa maji, hivyo basi siyo mkristo kabisa ni mkristo jina na mbinguni hauendi. MUNGU alileta ubatizo wa maji mengi na YESU pia na yeye alibatizwa ili kuonyesha njia. Sasa nawauliza ulimwengu, je hamuoni mmedanganywa na kupotezwa ingali mnampenda YESU lakini hamuelezwi ukweli ili mumfuate? Sasa uamue leo, ubatizwe ubatizo wa maji mengi uweke agano na YESU kuwa sasa wewe ni mkristo na ni mfuasi wake, umetimiza ahadi zako kwa kubatizwa kwa maji mengi.
Natumaini mnaelewa japo hata mimi iliniuma sana sababu nilidanganywa, nikaishi miaka mingi nikifikiri mimi ni mkristo salama kumbe nilikuwa ni mkristo mauti, ila neema yake ilinitoa nikawa mkristo hai na sasa nipo na YESU wa kweli kama mfuasi wake na mtumishi wake. Nawaeleza mumrejee MUNGU, mambo yameharibika kanisa limerudia yale ya Mafarisayo ya kulibadilisha neno la MUNGU na ndio sababu watu wamepotezwa. Neno linapobadilishwa tu uelewe ndio njia ya mbinguni imebadilishwa na kufuatwa njia ya jehanamu. Hivyo ikatae njia ya jehanamu sasa umeelewa YESU akija sasa sijui utakuwa katika eneo gani, wakati ndio sasa, hata hao wanaowabatiza watu kwa ubatizo ambao haupo katika biblia, hao pia siyo wakristo, huo ndio ukweli hata ukirudi katika neno la MUNGU, imeandikwa usiongeze neno wala kulipunguza (Ufunuo 22:18-19). MUNGU amekataa, sasa nyie wanadamu au makanisa je hamuoni mtahukumiwa kwa ajili ya hiki? Hata hiyo kazi na injili za jinsi hii nawatangazia mnapoteza muda wenu bali mnamfurahisha shetani kwa kutengeneza njia za kuwaangamiza watoto wa MUNGU waende jehanamu. Na ndiyo sababu nawaeleza kwa ujasiri kabisa hata ukisoma katika biblia utaona haupo na kama haupo basi umetokea wapi? Umeongezwa kwa kutoka kwa shetani. Shetani alitumia njia hii ili kuweka agano na wanadamu ili wawe watu wake kwa njia ya kuwabatiza watu kwa njia ya ubatizo wa kikombe, maji ya kisima, kuwabatiza watu kwa jina la mchungaji. Nawaeleza siri hii mfunguke ili mpone. YESU akija anaagalia agano lake. Sasa jiangalie wewe liko wapi agano lako la ubatizo aliobatizwa YESU? Jibu unalo peke yako.
Nawasihi mbatizwe upya na mkatengwe nao wala sehemu kama hizo penye agano la batizo za jinsi hiyo hapo hata siku moja hataonekana YESU WA NAZARETI hata kama jina lake linatajwa sababu hakuna agano lake la ubatizo wa maji mengi yanayotembea. Na kama umeshajua ukweli unasubiri nini? Je YESU akilinyakua kanisa lake sasa na wewe hauoni hautanyakuliwa sababu hauna agano la YESU WA NAZARETI bali unalo agano la shetani? Mrejee sasa utubu na yeye atakusamehe, na usishiriki katika maeneo ya jinsi hiyo sababu hakuna agano lake. Hata sadaka zako uelewe ulizipeleka kwa shetani na kila unapoenda hata katika makanisa ya jinsi hiyo uelewe unaenda kujihudhurisha mbele za shetani na siyo mbele za MUNGU.
Sema BWANA YESU naomba unisamehe, niandike jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele. Uniongoze nikabatizwe ubatizo kama uliobatizwa wewe pasipo kubadilishwa ili niingie agano na wewe, niwe mkristo wa kweli na siyo mkristo wa uongo tena. Amen.

 

NABII HEBRON



This post first appeared on UNABII WA KWELI, please read the originial post: here

Share the post

JE UNAJUA KAMA HUJABATIZWA KWA UBATIZO WA MAJI MENGI WEWE SIYO MKRISTO KABISA! SOMA HAPA UJUE UKWELI

×

Subscribe to Unabii Wa Kweli

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×