Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

MAKUFURU NI NINI?

BWANA YESU ASIFIWE!
Karibu Katika somo ambalo na kwenda kukufundisha mimi Nabii Hebron kama Mungu alivyonifundisha ili uelewe siri hii iliyofichika kuhusu kitabu cha ufunuo. Ukisoma katika kitabu cha Ufunuo 13:1-3 biblia inaelezea kuhusu makufuru makufuru na ukiendelea kusoma Ufunuo 13:1-7, 16…inaelezea vizuri zaidi.

MAKUFURU
Ni maneno mabaya yanayotolewa na Huyu Mnyama mwenye pembe kumi ambaye alipewa uwezo na joka kuu ili kutawala ulimwengu na kuwafanya wanadamu waweze kumtukana MUNGU pasipo wao kujua au kupenda japo wapo ambao wanajua kabisa wanamtukana MUNGU na wao wanapewa nguvu na huyu mnyama. Nitaelezea kwa ufupi; zaidi fuatilia YouTube ya Nabii Hebron na vitabu na kanisani yapo mafundisho yatakusaidia kuponywa nafsi yako.
Makufuru yapo ya aina mengi; nitaelezea 3…

1.     MAKUFURU YA KICHAWI
Makufuru haya ni maneno ambayo wachawi au washirikina huyasema wakati wakiwa katika kazi zao au matambiko vile vitu wanayoyafanya ndiyo makufuru na vitu vinatokea hao hupewa nguvu na huyo mnyama mwenye pembe kumi na kwa jinsi nyingine kila mchawi ni mwana chama wa namba 666, hata anayeendaga huko na yeye huwekewa namba 666 na huyo mnyama sababu ni roho zake ndizo zitendazo kazi sababu unamsujudia na yeye anakuwa ndiye mungu wako pasipo wewe kupenda wala kujua.
Watu wengi mmesikia kuwa watu wana wanga usiku, wengine wanapaa kwenye ungo, kulala makaburini, kuzini na waganga wa kienyeji, kuogeshwa na waganga wa kienyeji na mambo mengine yote unayofanyiwa nao pamoja na malipo; hayo malipo unakuwa umempa sadaka huyo mnyama na pia unakuwa na wewe unaunganishwa katika kumtukana MUNGU kwa sababu hayo unayoyashiriki siyo yake, hayapo katika biblia na ukisoma katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana 22:18-20 MUNGU alikataa yasifuatwe tofauti na alivyoandika katika kitabu chake, ila yeye alijua habari ya huyu mnyama mwenye pembe 10 na vichwa vyake ataleta maneno mabaya (makufuru) ili atukanwe MUNGU kwa matendo unayoyafanya au kuvunja amri zake.
2.     MAKUFURU YA MITAMBIKO
Mitambiko yote ni ibada za shetani na yanapofanyika  anatukuzwa huyu mnyama kwa sababu unakuwa umemfuata huyu mizimu wakati huo  na kisha unaenda kanisani, hapo wewe unakuwa ni mnafiki mbele za MUNGU bali Bwana wako anakuwa huyu mnyama  katika ulimwengu wa roho pasipo wewe kujua wala kupenda na unakuwa unayo namba 666. Hivyo ni vizuri uombewe, utubu na uache hiyo namba 666 ikutoke kwa jina la YESU WA KWELI kwa sababu yupo yesu wa uongo pia; yeye yupo chini ya huyu mnyama aliyepewa amri ya kuwateka wanadamu ambaye ndiye mpinga kristo na kusababisha katika ulimwengu huu kumetokea ukristo wenye mbili ambao ni ukristo wa kweli na ukristo wa uongo.

3.     MAKUFURU YA UKRISTO WA UONGO YAKOJE?
Kila kiumbe kinajua kuwa YESU yeye ndiye njia ya uzima na kweli na yeye ndiye Nabii ambaye ameteuliwa na MUNGU aliyeumba vitu vyote ya kuwa ndiye atakayekuja katika unyakuo na katika kutoa hukumu ya kiama au kwa lugha nyingine anaitwa Nabii Issa. Hapa ndipo lilipoanza chimbuko la kuongezeka ukristo wa pili ambaye ndiye wa uongo upo tofauti na lilivyo neno la MUNGU likachanganywa na uongo, ikawa injili ya namna nyingine soma Wagalatia 1: 6-9 na injili hiyo ya tofauti inawafanya watu wanaoipokea walaaniwe. Makufuru haya ndiyo maneno ya kumtukana MUNGU pale yanapochanganywa na neno la kweli au kutumia biblia ikisomwa kanisani halafu mmeamua kuchangisha pesa katika nyumba ya sala au ili uombewe unadaiwa pesa kwanza umpe pastor ndiyo maneno ya kumtukana MUNGU sababu yapo kinyume na yeye, siyo yake. Utajiuliza sasa mbona hayapo katika biblia sasa yanatokea wapi na ni wapo shina lake au mafunuo hayo yanatokea wapi na yapo kinyume na neno la MUNGU.
Ukisoma katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana 22:18-20 inaonya usiongeze neno lolote; MUNGU akijua huyu mnyama ataleta injili yake ya tofauti ataichanganya neno lake; hapa mwenye akili na aelewe. Siyo kila mtumishi anayesoma biblia kanisani anatumiwa na MUNGU, wengi zaidi wameongozwa na huyu mnyama na tayari wanazo namba 666 na wewe muumini unapoabudu hapo namba hiyo inakugonga katika ulimwengu wa roho pasipo wewe kujua wala kupenda kwa sababu ya matendo haya:
1.     Ubatizo wa kikombe, ubatizo wa kisima, kubatizwa kwa jina la mchungaji. Ubatizo wa kisima; unaweza kisima kukaa karibu na madhabahu ndani au likawa nje ya kanisa. Hili ni kufuru la huyo mnyama na hapo umepokea ubatizo wa makufuru haujatokea kwa MUNGU. Je umetokea wapi? Haijulikani. Hivyo yule mnyama ndivyo anavyomuaga hizo za batizo tofauti na biblia na watumishi baadhi wakatawaliwa na namba 666.
2.     Kuomba michango ya TV, radio, imeadikwa usifikirie nini nitatenda; unapoona hivyo uelewe ni ile roho ya mnyama hayo ni maneno mabaya ya kuharibu ahadi za MUNGU
3.     Kuandika sadaka majina, kupewa risiti, kusomwa jina umetoa vizuri; unapewa cheti cha hongera unakuwa mtoaji bora. Ni makufuru ya huyo mnyama na ndiye anayewapa nguvu na hii inawafanya ulimwengu kutekwa na shetani 98% kwa sababu ya makufuru ya huyu mnyama.
4.     Huduma zenye kuongozwa na huyu mnyama, kuhani anakuwa ni mzinzi  kisiri au hata kiwazi wazi bila hofu; pasipo kuangushwa na shetani katika dhambi ya uzinzi, anakuwa ni mlevi, anajisifia sana, anatenda miujiza ya kipepo, anaweka bendera au kujenga minara yake; ile minara ni vichwa vya huyu mnyama vinampa mawasiliano ya nini cha kufanya, wengine wapo katika chama cha freemason hata sasa majina yao yapo waziwazi. Habari zaidi ni pesa na mengineyo ambayo hayampendezi MUNGU hufanyika hapo. Zaidi hupenda kufanya maagano ya makafara ya uzinzi, kuosha waumini miguu badala ya watumishi wa MUNGU.
NOTE:

Yapo mengi ila zaidi endelea kusoma blog hii na kutumia wengine wapate kusoma ili wasiongozwe tena na makufuru ya huyu mnyama.

Mrejee YESU wa kweli; sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote, hata pale nilipokutukana wewe MUNGU wangu kupitia kuyatenda mambo yasiyokupendeza wewe au kupokea mafundisho kinyume na sheria zako. Ninamkataa huyu mnyama mwenye vichwa 10 na mambo yake yote ya uongo yanayompinga kristo. Futa jina langu kwenye kitabu cha hukumu andika jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele. Nakupenda BWANA YESU, niongoze mahali ambapo hakuna makufuru, mahali ambapo wewe MUNGU wa kweli upo. Amen.
MUNGU AKUBARIKI.

NABII HEBRON.


This post first appeared on UNABII WA KWELI, please read the originial post: here

Share the post

MAKUFURU NI NINI?

×

Subscribe to Unabii Wa Kweli

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×