Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

TAWA yaitikia wito wa Rais Samia, yazichangia milioni 10 Serengeti Girls,Tembo Warriors

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Mamlaka ya Usimamizi wa Wanayamapori Tanzania (TAWA) imechangia kiasi cha Sh milioni 10, ikiwa ni kuitikia wito wa Rais Samia Suluhu Hassan wa kuzisaidia timu za Serengeti Girls na Tembo Warriors ambazo zinapaswa kushiriki michuano ya kimataifa huko India na Uturuki.

Uchangiaji wa fedha hizo uliongozwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika kikao maalumu kilicho fanyika jijini Dar es Salaam ambacho kimewashirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo ya michezo kwa lengo la kujadili na kuchangia timu hizo.

Miongoni mwa wadau ambao wamechangia Katika Kikao Hicho ni pamoja Mamlaka hiyo ya Usimamizi wa Wanyama pori(TAWA) ambao kupitia kwa Afisa Mahusiano, Vicky Kamata kwa niaba ya Kamishna wa uhifadhi amesema wameamua kuunga mkono juhudi la Rais katika kuendeleza michezo nchini.

Kiasi hicho cha pesa kitasaidia kuwapa motisha timu zote mbili ya wanawake wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Girls) na timu ya wenye ulemavu (Tembo Warriors) kujiandaa vyema kwa ajili ya mashindano ya kimataifa.

Jumla ya fedha zilizopatikana katika kikao hicho ni shilingi Billioni 1.26 ambazo zitawawezesha kuelekea nchini Uingereza katika jiji la Southampton kwa ajili ya maandalizi ya michuano hiyo.

The post TAWA yaitikia wito wa Rais Samia, yazichangia milioni 10 Serengeti Girls,Tembo Warriors appeared first on News Africa Now.



This post first appeared on News - News Africa Now, please read the originial post: here

Share the post

TAWA yaitikia wito wa Rais Samia, yazichangia milioni 10 Serengeti Girls,Tembo Warriors

×

Subscribe to News - News Africa Now

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×