Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Tanzania yaanza vibaya Kombe la Netiboli Afrika

Na Mwandishi Wetu

TIMU ya Taifa ya Tanzania ya Netiboli, Taifa Queens, imeanza vibaya michuano ya Kombe la Netiboli kwa nchi za Afrika baada ya kufungwa na Uganda ‘She Cranes’, magoli 77-29 katika mchezo wa ufunguzi, uliochezwa leo asubuhi Novemba 9, 2021 kwenye Uwanja wa Wanderers Sports Arena, Windhoek, nchini Namibia.

Katika mchezo huo, Taifa Queens Imeanza robo ya kwanza kwa kufungwa magoli 20-7,robo ya pili 22-7, robo ya tatu 18-7 na robo ya nne 17-8.

Michuano hiyo inayoendelea nchini Namibia, inatarajia kufikia tamati Novemba 16,2021 ikishikisha jumla ya timu tisa ambazo ni mwenyeji Namibia, Botswana, Zambia, Zimbabwe, Tanzania, Kenya, Uganda, Malawi na Afrka Kusini.

The post Tanzania Yaanza Vibaya Kombe la Netiboli Afrika appeared first on News Africa Now.



This post first appeared on News - News Africa Now, please read the originial post: here

Share the post

Tanzania yaanza vibaya Kombe la Netiboli Afrika

×

Subscribe to News - News Africa Now

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×