Wakulima Same Kuanza Kulima Zao la Jatrofa
2008-01-31 13:58:20
Na ITV Habari
Baadhi ya wakulima wa wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro wamehamasika na kuanza kulima zao la Jatrofa baada ya mafuta ya zao hilo kuanza kutumika kuendeshea injini za magari.
Wakizungumza baada ya kuona gari linalotumia mafuta yanayotokana na zao hilo wakulima hao wamesema wamepata matumaini makubwa ya kuondokana na umaskini kupitia zao hilo jipya la biashara.
Naye mwakilishi wa shirika linalotengezeza mafuta hayo kutoka nchini Uholanzi Bw. Adjan Deoswijk amesema mafuta hayo ambayo pia hutumika kwenye mashine za kuzalisha umeme zikiwemo genereta yameonyesha uwezo mkubwa wa kuendesha injini za magari.
* SOURCE: ITV