Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Harmonize atimka baada ya kukutana na meneja wa Harmorapa kwenye kipindi


Muimbaji wa WCB, Harmonize ilikuwa awepo kwenye kipindi cha FNL cha Televisheni Ijumaa hii, lakini ameingia mitini baada ya kumuona meneja wa msanii Harmorapa maeneo ya studio hizo. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na EATV kupita twitter, zinadai kuwa baada ya Harmonize kumuona meneja wa Harmorapa, msanii huyo amemuoneshea kidole cha kati ambacho hudaiwa kuwa ni ishara ya tusi kisha akaondoka maeneo ya studio hizo. “Tunaomba radhi kwa ishara aliyoionesha hapa na Hamorappa wakati akielezea kitendo kilichofanywa na Harmonize,” walitweet EATV. Harmorapa akiongea katika kipindi hicho, amelaani kitendo hicho cha udharirishaji na kudai kuwa Harmonize amemtukana bosi wake kwa kumuonyesha ishara ya kidole cha kati baada ya kukutana. “Kwa kweli sijapenda Harmonize amemtukana bosi wangu kwa kumuonesha kidole cha kati, sijapenda kabisa,” alisema Harmorapa. Kwa upande wao, kituo cha EATV, kupitia Twitter kimeomba msamaha kwa watazamaji wake wote kutokana na kitendo hicho cha aibu kilichofanywa na msanii huyo.


This post first appeared on HABARI ZA SIASA NA MUZIKI, please read the originial post: here

Share the post

Harmonize atimka baada ya kukutana na meneja wa Harmorapa kwenye kipindi

×

Subscribe to Habari Za Siasa Na Muziki

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×