Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Mwanjali Kuongeza Nguvu Leo Simba Ikianza Mazoezi Leo

WAKATI Simba leo wakianza Mazoezi baada ya mapumziko ya siku mbili, habari njema kwa mashabiki wa timu hiyo ni Kurejea Kwa Beki mkongwe, Method Mwanjali.
Mwanjali leo anatarajia kuanza mazoezi ya pamoja na wachezaji wenzake baada ya kuthibitishwa kupona majeraha yake.
Kocha wa timu hiyo, Joseph Omog, aliiambia Nipashe jana kuwa ni jambo jema kurejea kwa beki huyo ambapo alisema itampa wigo mpana wa kuamua mchezaji wa kucheza.
"Tunaanza mazoezi kesho (leo) na tutakuwa na programu maalum kuelekea kwenye michezo yetu mitatu ya ugenini, nafurahi kurejea kwa Mwanjali kwa sababu atakiimarisha kikosi chetu," alisema Omog.
Alisema kuwa kabla ajaanza mazoezi ya pamoja na wenzake atampa programu maalum ya kumrejesha kwenye mazoezi ya nguvu beki huyo wa kati.
Simba inajiandaa kwa ajili ya michezo yake ya kanda ya ziwa dhidi ya Kagera Sugar (Aprili 2), Mbao FC (Aprili 6) na Toto African Aprili 12.
Vinara hao wa Ligi Kuu wamepanga kuanza mazoezi kwenye uwanja wa Chuo cha Polisi, Kurasini jijini Dar es Salaam ambako pia kwa nyakati tofauti Yanga imekuwa ikiutumia Uwanja huo kwa mazoezi yao.



This post first appeared on HABARI ZA SIASA NA MUZIKI, please read the originial post: here

Share the post

Mwanjali Kuongeza Nguvu Leo Simba Ikianza Mazoezi Leo

×

Subscribe to Habari Za Siasa Na Muziki

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×