Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Wanahabari Watatu Wauawa Ndani Ya Mwezi Huu Mexico

Ujumbe ulioachwa baada ya kuuawa kwa Mirosalva Breach umeonyesha wauaji walichukizwa na Ripoti zake
Muandishi wa habari nchini Mexico ameuawa kwa kupigwa risasi katika jimbo la Chihuahua, yeye ni mwana habari wa tatu kuuawa nchini humo mwezi huu.
Mirosalva Breach alipigwa risasi akiwa ndani ya gari lake nje ya makazi yake mjini Chihuahua.
Mmoja wa watoto wake ambaye alikuwa naye ndani ya gari, hakujeruhiwa.
Watu wenye silaha waliacha ujumbe uliosema '' kwa kuwa na mdomo mrefu''.
Bi Breach aliripoti kuhusu masuala ya uhalifu, biashara ya dawa za kulevya na rushwa katika gazeti la kitaifa, mjini humo La Jordana na Notre de Juarez.
Kamati inayotetea waandishi wa Habari imesema wanahabari 38 wameuawa nchini Mexico tangu 1992.



This post first appeared on HABARI ZA SIASA NA MUZIKI, please read the originial post: here

Share the post

Wanahabari Watatu Wauawa Ndani Ya Mwezi Huu Mexico

×

Subscribe to Habari Za Siasa Na Muziki

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×