Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Kuhusu Nape Nnauye, CUF kutangaza hatua nzito

TAARIFA KWA UMMA NA VYOMBO VYA HABARI
Chama cha Wananchi CUF kimepokea taarifa ya hatua ya Rais Magufuli kufanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri na kumuondoa Mheshimiwa Nape Nnauye katika nafasi ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, kwa mshtuko na masikitiko makubwa.
Mhe. Nape ameondolewa kwenye Baraza la Mawaziri kibabe na bila aibu kutokana na kusimamia Haki, Uhuru, Uwajibikaji, Nidhamu na Maadlili ya uendeshaji wa vyombo vya habari nchini jambo ambalo ni jukumu la msingi la Wizara yake.
Sote tunatambua kwamba Utenguzi huo unatokana na Mhe. Nape kufuatilia tukio la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuvamia kituo cha Clouds Media Group kinyume na taratibu, maadili na Nidhamu ya utendaji wa majukumu yake. kitendo hicho pia ni kosa la jinai lisilovumilika.
Kwa niaba ya Chama cha Wananchi CUF, napenda kutumia fursa hii kulaani mwenendo wa Rais Magufuli wa kuitumia nafasi yake kwa namna inayokosa BUSARA na HEKIMA ya uongozi kwa TAASISI ya URAIS.
Kitendo cha Rais kumlinda mtuhumiwa ambaye amefanya makosa ya wazi kabisa kinadhihirisha namna Rais asivyo na utayari wa dhati na uwezo wa kusimamia nidhamu ya watendaji serikalini.
Huko nyuma na mara kadhaa, Rais Magufuli alichukua hatua za haraka sana kuwafuta kazi watumishi na watendaji wa serikali waliofanya makosa madogo mno hata kama ilikuwa ni kimatamshi tu au maamuzi ya bahati mbaya.
Mifano mizuri ni pamoja na Mhe. Anne Killango (aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga), Dr. Mwele Malecela (aliyekuwa anaongoza taasisi muhimu ya utafiti wa magonjwa ya binadamu), Wilson Kabwe (Mkurugenzi wa Jiji la Dar Es Salaam) ambaye alituhumiwa mkutanoni na kufukuzwa hapo hapo bila kuwepo wala nafasi ya kujitetea.
The Civic United Front (CUF) inashangazwa na maamuzi ya sasa ya Rais Magufuli ya kumlinda mtuhumiwa wa makosa makubwa na ya wazi kabisa na kisha kumfukuza kazi Waziri aliyekuwa akitekeleza wajibu wake ili kulinda heshima ya serikali.
Kwa kitendo hiki cha Rais, CUF inaungana na watanzania wote kuamini kuwa Rais Magufuli hana nia njema ya kurejesha nidhamu serikalini, na kwamba yuko tayari kuwalinda vijana wake wachache kuliko kuilinda serikali na heshima ya nchi na Taasisi ya Urais. Rais anashusha hadhi ya Ikulu na sasa ikulu imegeuka kuwa mtetezi mkuu wa watumishi waovu wa umma.
CUF itatangaza hatua nzito hapo baadaye, kwa niaba ya chama natumia fursa hii kumfariji na kumtia nguvu Mhe. Nape kwa ujasiri aliouonyesha na kusimamia kile ambacho ni haki kwa Taifa, wananchi na sekta ya habari.
Namuomba asirudi nyuma kutetea haki za watanzania wote na kamwe asikatishwe tamaa na kitendo hicho kilichokosa utu na heshima, na kujali mchango mkubwa wa kisiasa ndani ya Chama chake na serikali ya awamu ya Tano.
CUF inaungana na watanzania wote kulaani kitendo hicho na kwamba tutakutana pia na vyama washirika katika UKAWA ili kuamua hatua kubwa za pamoja dhidi ya ukosefu wa haki na Demokrasia nchini na matumizi mabaya ya mamlaka.
"CUF NI TAASISI IMARA YENYE VIONGOZI MAKINI"
HAKI SAWA KWA WOTE
JULIUS MTATIRO
MWENYEKITI WA KAMATI YA UONGOZI
CUF-TAIFA.
23 Machi, 2017.



This post first appeared on HABARI ZA SIASA NA MUZIKI, please read the originial post: here

Share the post

Kuhusu Nape Nnauye, CUF kutangaza hatua nzito

×

Subscribe to Habari Za Siasa Na Muziki

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×