Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Mapato ya mchezo wa Madini na Simba yang'oa kigogo Arusha

Arusha .Meneja wa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha, Jackson Jolwa amesimamishwa kazi na wammiliki wa uwanja huo kwa madai alikuwa hafanyi ipasavyo majukumu yake.
Katibu wa siasa na uenezi wa CCM, Shaaban Mdoe alisema uongozi wa chama hicho ulimsimamisha baada ya mechi ya Madini dhidi ya Simba iliyofanyika uwanjani hapo.
“Wengi wanasema tumemsimamisha kutokana na mapato ya mchezo ule lakini, kinachotakiwa kujulikana kuwa CCM wanapata asilimia 15 ya mapato kwa chochote kinachofanyika hapa, na zoezi hilo husimamiwa na idara ya uchumi,” alisema Mdoe.
Aliongeza kuwa na zoezi la kusimamia mapato kwenye mchezo huo lilipaswa kufanya na mchumi wa chama hicho ambaye siku ya mchezo hakuwepo ndipo aliteuliwa yeye Shaaban Mdoe kulisimamia hilo na siyo kazi ya meneja kusimamia mapato yale.
Akizungumza madai hayo Jackson Jolwa alisema hakuna kosa alilolifanya bali ni ugomvi wao binafsi ndio umesababisha hadi kusimamishwa kazi.
Alisema tatizo hilo lilianza siku ya mchezo wa Madini dhidi ya Simba ambapo katibu mwenezi huyo alitaka aweke vijana wake wasimamie mapato jambo alilipinga kwa madai siyo kazi yao.



This post first appeared on HABARI ZA SIASA NA MUZIKI, please read the originial post: here

Share the post

Mapato ya mchezo wa Madini na Simba yang'oa kigogo Arusha

×

Subscribe to Habari Za Siasa Na Muziki

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×