Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Waziri Ajiuzuru Nchini Ufaransa

Waziri wa mambo ya ndani wa Ufaransa,Bruno Le Roux, amejiuzulu, baada ya kuibuka shutuma Kuwa aliwaajiri Binti Zake wawili kuwa wasaidizi wa bunge wakiwa wanafunzi.
Waendesha mashtaka walifanya uchunguzi wa awali kuhusu mikataba yenye thamani ya karibu dola elfu sitini ambazo bwana Le Roux aliwapa binti zake kati ya mwaka 2009 na mwaka 2016.
Amesema hakuna sheria ya bunge iliyokiukwa na watoto wake walifanya kazi kwa uhalali, lakini hakutaka kuwa kikwazo kwa Serikali.
Wakati huohuo, uchunguzi kama huo umeendelea kufanyika dhidi ya mgombea urais kutoka chama cha Conservative Francois Fillon, ambaye anashutumiwa kufanya udanganyifu.
Fillon amekana kuajiri familia yake na kuwalipa mishahara minono, kashfa ambayo imetia dosari mchakato wake wa kuwania urais



This post first appeared on HABARI ZA SIASA NA MUZIKI, please read the originial post: here

Share the post

Waziri Ajiuzuru Nchini Ufaransa

×

Subscribe to Habari Za Siasa Na Muziki

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×