Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Mkude: Tunamzuka na makombe mawili

NAHODHA wa Simba, Jonas Mkude, amesema mzuka wa kutaka kuchukua Makombe Mawili unazidi kuwapanda kichwani wachezaji wa timu hiyo na wamepania kutimiza lengo hilo.
Akizungumza na Nipashe jana, Mkude alisema ushindi wa bao 1-0 walioupata kwenye mchezo wao wa robo fainali dhidi ya Madini FC ya Arusha Jumapili iliyopita, umewafanya kuona wanakaribia kutimiza ndoto hiyo.
"Hiki ndicho kitu ambacho kipo akilini mwetu, tutapambana kuona tunafikia malengo na ndoto yetu ya kutwaa makombe mawili msimu huu, nia hiyo tunayo," alisema Mkude.
Alisema changamoto iliyopo mbele yao kwa sasa ni michezo yao ya Kanda ya Ziwa ambayo wanaamini kama watafanikiwa kufanya vizuri watakuwa wameukaribia ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu.
Wakati wakiwa wanaongoza msimamo wa Ligi Kuu kwa tofauti ya pointi mbili, Simba tayari imetinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho (FA)



This post first appeared on HABARI ZA SIASA NA MUZIKI, please read the originial post: here

Share the post

Mkude: Tunamzuka na makombe mawili

×

Subscribe to Habari Za Siasa Na Muziki

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×