Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

WANAYOPASWA KUFANYA WENYE VVU KUEPUKA MARADHI YA KINYWA


Watu wengi walioathiriwa na Virusi Vya Ukimwi (VVU), hupatwa na maradhi tofauti ya kinywa.

Na wakati mwingine wanapopatiwa matibabu ya kinywa na madaktari, huwa hawasemi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya usiri wa mgonjwa kwa daktari kuhusu afya yake kwa ujumla, kukosa umakini kwa daktari ama sababu nyingine yoyote.
Hivyo, kushindwa kutambua hali hii, husababisha mhusika kukosa matibabu sahihi, hivyo kuendelea kuumia.

Kwa maana hiyo, ni muhimu kwa waathirika kufahamu ya kwamba, wanapokwenda kwa daktari wa kinywa na meno kupatiwa tiba, ni vyema wakaelezea historia nzima ya afya zao.

Hii itamsaidia daktari kupata ufahamu wa kutosha na kumuwezesha kutoa matibabu husika na kikamilifu.

Kwani baadhi ya maradhi yanayoweza kumkumba muathirika wa ukimwi kinywani ni pamoja na kinywa Kuwa kikavu (Xerostomia), fangasi (candidiasis), maradhi ya fizi (Periodontal diseases), saratani ya kinywa na vidonda kinywani.

Ila izingatiwe maradhi niliyoyataja hapo juu si kwamba huugua watu wenye maambukizi ya VVU au wanaougua Ukimwi pekee la hasha, yanaweza kumpata yeyote yule.

Ila muathirika yuko kwenye hatari ya kuugua mara kwa mara kutokana na kupungua kwa kinga ya mwili.

Madhara

Madhara ya aina mbalimbali huweza kuwakumba waathirika wa VVU/Ukimwi kwa asilimia 30 hadi 80 kama hawatayatibu haraka.
Hiyo husababishwa na ukimya wa wao kutotoa taarifa kwa madaktari wanaokwenda kutibiwa.

Utafiti uliofanyika kwa nchi zilizoendelea unaonesha asilimia 9.1 tu ya waathirika ndiyo hupata matibabu sahihi ya maradhi hayo ambayo hutokea kinywani ikiwa ni matokeo ya maambukizi ya VVU na kuugua Ukimwi.

Hata hivyo, inaelezwa maradhi hayo ya kinywa yameanza kupungua kwa waathirika tangu yalipoanza matumizi ya dawa za kufubaza virusi.

Tatizo la kinywa kikavu

Hali ya kinywa kuwa kikavu inayosababishwa na kupungua kwa uzalishaji wa kawaida wa mate, ni moja kati ya sababu kuu zinazochangia kutoboka kwa meno kwa waathirika wa VVU/Ukimwi.

Inakadiriwa asilimia 30 hadi 40 ya waathirika wa virusi vya ukimwi na ukimwi, hupitia hali hiyo ya kuwa na kinywa kikavu cha hali ya wastani hadi ya juu, hali ambayo husababishwa na baadhi ya dawa za kufubaza makali ya VVU/ukimwi ikiwamo aina ya didanosine, au husababishwa na kuongezeka kwa seli za CD8+ kwenye matezi makubwa ya kuzalisha mate kinywani.

Mabadiliko ya wingi na ubora wa mate ikiwamo wa kupambana na bakteria kinywani, huweza kusababisha pia kuoza kwa meno miongoni mwa waathirika wa virusi vya Ukimwi na pia kusababisha mardahi ya fizi miongoni.

Fangasi wa aina gani huwakumbwa waathirika wa VVU na Ukimwi.

Fangasi wa kwenye kinywa huweza kutokea katika sura mbalimbali kama vile vidonda sugu kwenye kona za midomo ama hali ya utando mweupe usioondoka kwa kupiga mswaki ama kukwangua kwa ulimi.

Halikadhalika, kuna aina nyingine ya fangasi ambayo huwa ni ngumu kuitambua kitaalamu inaitwa Erythematous candidiasis.
Hizi ni fangasi ambazo mara nyingi huwatokea zaidi watu walioathirika.

Mgonjwa hutokewa na alama nyekundu inayosambaa kidogo na kutengeneza duara kwenye sehemu ya juu ya ulimi ama kwenye kaakaa.

Mgonjwa mwenye hali hii huwa analalamika kupata maumivu kila alapo vitu au vyakula vyenye chumvi, pilipili au kunywa vitu vyenye vya asili ya tindikali.

Fizi kuvimba na kutoa damu

Ugonjwa wa fizi kutoa damu husababishwa na kuvimba.  Mara nyingi ufizi wenye kutoa damu.  Na mara nyingi huwa na rangi nyekundu tofauti na rangi ya kawaida ya pinki ya ufizi wenye afya.
Kwakua ugonjwa huu hasa katika hali ya mwanzo unaweza usionekane kama ni tatizo, lakini inapaswa itambulike kuwa ufizi wenye afya njema hautoi damu wakati wa kupiga mswaki ama uking’ata kitu, hivyo ni muhimu kuchukua hatua mapema ili kuutibu.

Hii ni kwa sababu ugonjwa huo unapoendelea huweza kuathiri mfupa wa taya sehemu ambayo jino hujishika.  Ikiachwa pia huweza jino ama meno kulegea na hata kung’oka.

Wakati ni kweli kuwa ugonjwa wa fizi kuvimba na hata kutoa damu huweza kumpata mtu yeyote yule ambaye hazingatii misingi ya afya bora ya kinywa, kwa waathirika wa ukimwi hali hii huwatokea zaidi kutokana na kuwa na kinga dhaifu ya mwili.

Ufizi wenye afya ni imara na una rangi ya pinki iliyopauka.  Kama fizi zimevimba, zimekuwa nyekundu na zinatoa damu kiurahisi inawezekana mhusika ana tatizo la ugonjwa wa fizi.  Na kwa kuwa ugonjwa huo mara nyingi hauna maumivu, unaweza kudumu kwa muda mrefu bila kujijua.

Dalili zake ni zipi

Dalili zake ni pale mtu anapobaini kuwa fizi zake zimevimba, kulainika na kuanza kubonyea.

Wakati mwingine mgonjwa hujihisi fizi hizo zinamuuma au kutoa damu kirahisi mara anapopiga mswaki au anapoflosi na wakati mwingine anaweza kutoa damu kwenye mswaki.

Dalili nyingine ni mabadiliko ya rangi ya ufizi kubadilika na kutoka rangi ya pinki iliyopauka na kuwa nyekundu sambamba na harufu mbaya ya kinywa.

Kaposi sarcoma

Huu ni aina ya uvimbe unaoambatana mara nyingi na maambukizi ya virusi vya ukimwi na huweza kutokea sehemu yoyote ya mwili, hata hivyo hutokea mara nyingi kinywani kuliko sehemu nyingine.
Uvimbe huo huwa na rangi mbalimbali ikiwamo nyekundu na zambarau na kimaumbile, huweza kuwa na sura ya ama kinundu, ama kidonda ama hata kiduara cha rangi ya zambarau ama nyekundu bila kuwa na uvimbe.

Kwa kawaida uvimbe huo hauna dalili yoyote ya maumivu na rangi yake huzidi kukolea kadiri muda unavyoongezeka.

Vidonda vya mara kwa mara

Hivi ni vile vinavyotokea kinywani na kwa kawaida hujirudia mara kwa mara hata baada ya kupona.

Halikadhalika, vidonda hivyo huweza kutokea sehemu yoyote ya kinywa.  Mpaka sasa sababu ya kwa nini vinatokea haijajulikana.  Lakini inahusishwa na kupungua kwa kinga mwilini.

Ikumbukwe vidonda hivyo huweza kumtokea hata mtu asiye na maambukizi na vina dalili sawa.  Inaaminika kuwa msongo wa mawazo ama madabadiliko ya vichocheo (hormone) ambayo hushusha kinga ya mwili husababisha mtu kuugua.

Vidonda hivyo huwa vinauma hasa wakati wa kutumia vyakula vya chumvi, pilipili ama vinywaji vyenye asili ya tindikali.

Kwa mtu ambaye hajaathirika vidonda hivyo vinaweza kudumu kwa siku kati ya saba hadi 14 kupona, lakini kwa muathirika huchukua muda mrefu zaidi.

Madhara ya hali hiyo kinywani

Hali hii ya maradhi mbalimbali kinywani miongoni mwa wagonjwa au waathirika wa ukimwi huwa na athari za moja kwa moja kwa afya zao.

Kwani pamoja na mambo mengine, huweza kusababisha yafuatayo madhara kwa mhusika ikiwamo kukosa hamu ya kula, kwani wengi wao huona kula chakula ni kama sehemu ya adhabu kutokana na maumivu anayoyapata wakati wa kula.

Wengi hukata tamaa ya kuishi anapoona hawezi kula kama kawaida, hali hii humsababishia kudhoofu afya yake na kuhatarisha maisha yake.

Kwani kama mtu anatumia dawa za kufubaza virusi vya ukimwi halafu hapati lishe ya kutosha, matokeo yake ni kumpoteza.


This post first appeared on Afya Na Kiasi, please read the originial post: here

Share the post

WANAYOPASWA KUFANYA WENYE VVU KUEPUKA MARADHI YA KINYWA

×

Subscribe to Afya Na Kiasi

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×