Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

MAZOEZI MEPESI HUTOA MARADHI NYEMELEZI


Nikiwa mmoja wa waunga mkono katika juhudi za kukabiliana na magonjwa yasiyoambukiza yaani non-communicable disease leo nitawapa dondoo zinazohusu Mazoezi mepesi.

Kama ilivyoendelea kuelezwa na serikali kuwa kutakuwa na utaratibu wa kufanya mazoezi kila Jumamosi ya pili ya mwisho wa mwezi.  Ninafahamu wengi wanaweza kujitokeza lakini je wanajua ni kwa muda gani wafanye mazoezi yawe ya aina gani.

Ieleweke kuwa mazoezi yanayotakiwa kufanywa ni Mazoezi Mepesi kitaalamu hujulikana kama aerobic exercise.

Mazoezi mepesi ni pamoja na kukimbia mbio za taratibu, kutembea, kuogelea, kuruka Kamba, kufanya kazi ndogo ndogo, kuendesha baiskeli na kucheza mziki.

Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali zimebaini kuwa mazoezi mepesi ndiyo yanayochangia watu kuishi maisha marefu zaidi.  Hii ni hutokana na mazoezi haya kumuepusha mtu na magonjwa ya moyo, kisukari, shinikizo la damu na unene uliopitiliza.

Mazoezi haya kama yakifanywa kwa ufanisi ndiyo silaha bora ya kukabiliana na magonjwa yasiyoambukiza ikiwamo kisukari, magonjwa ya moyo na unene uliopitiliza.

Mazoezi mepesi hayahitaji kwenda katika vituo vya mazoezi vya kulipia, yanafanyika katika maeneo ya wazi na njia za watembea kwa miguu.

Faida ya mazoezi haya ni pamoja na kuchoma mafuta yaliyorundikana, kuimarisha afya ya moyo na mapafu hivyo kukufanya kuwa na upumuaji mzuri na mzunguko imara wa damu.
Vilevile hukusaidia kukupa mwili makakamavu na utulivu wa kiakili na kimwili.

Mazoezi haya yanakufanya kuepukana na msongo wa mawazo ambalo ni moja ya magonjwa yasiyoambukiza.

Wataalam wa sayansi ya michezo wanashauri mazoezi mepesi yafanyike angalau mara tano kwa wiki, kwa siku iwe kwa dakika 30-40.

Muda huu ndiyo unakubalika na wanasayansi wa michezo kuwa unaufanya mwili kutumia mafuta yaliyorundikana.

Kama ni kutembea umbali unaopendekezwa kitaalam ni kilomita 2 kwa siku.  Mazoezi mepesi yana ufanisi zaidi kama yakifanywa nyakati za jioni au asubuhi.

Pale unapofanya mazoezi kila mara na kwa muda mrefu ndivyo pia mwili unatumia zaidi mafuta yaliyorundikana hivyo kuwezesha kudhibiti unene/uzito mkubwa.

Hivyo kuanzishwa kwa utaratibu wa kufanya mazoezi kila Jumamosi ya pili ya mwezi na Serikali ichukuliwe kuwa ni kichochezi cha kutufanya kupenda kufanya mazoezi mepesi.


Isije ikatokea kuwa unafanya tu mazoezi hayo katika siku hiyo tu ilyoelekezwa, utakuwa unajidanganya kwani ili kuweza kupata afya njema inahitajika kujenga tabia ya kufanya mazoezi mepesi mara kwa mara kwa muda mrefu. 


This post first appeared on Afya Na Kiasi, please read the originial post: here

Share the post

MAZOEZI MEPESI HUTOA MARADHI NYEMELEZI

×

Subscribe to Afya Na Kiasi

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×