Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

IBADA: MAADILI SITA KWA NYUMBA YA KIKRISTO YENYE AFYA

Tags: kuwa katika kama

Nyumba ya kikristo ni mahali pa muhimu sana ambapo tunakamilishana kila mmoja na mwenzake.  Ni Katika hali hii kwamba wanafunzi wawili wa Biblia ambao wanafahamika sana walisema wakati Fulani Kuwa nyumbani hapakukusudiwa kuwa mahali ambapo mtu anakamilika kama mtu.  Mtu anamhitaji mwingine ili kuwa kamili.

Kwa nyumbani kukamilisha kitu cha thamani kuu kama hiki kunahitaji kuwa mahala salama kwa sababu kumetengwa kuwa sehemu salama kukuza maadili kwa nyumba ya kikristo yenye afya.


Kamusi ya kiingereza ya Collins iliyo chapishwa mwaka 2003 inalifasili neno maadili kama hali ya kuwa na shauku ya kitu mara nyingi kuhusiana na rasilimali kama vile matumizi yake au ubadilishano: kufaa, stahili au umuhimu sahihi.  Kwa namna nyingine maadili yanaweza yakafasiliwa kama kanuni ya maadili na imani au kipimo kilicho kubalika cha mtu au kikundi cha kijamii.  Hivyo, maadili yametolewa au yameanzishwa  yawe pale ili yaweze kusaidia kujenga maisha ya Kikristo, ya kifamilia, na ya kinyumba.

Biblia katika kitabu cha Mwanzo 2:18 inathibitisha kuwa inachukua wawili kumfanya mmoja.  Bwana akasema “Si vema mtu awe peke yake---” kwa hiyo upweke haukuwa katika mpango wa Mungu kwa afya ya maisha yetu ya kifamilia.  Swali ambalo mtu anaweza akajiuliza mwenyewe ni hili kwa nini wawili na sio watatu?

Maisha ya mume na mke ni klabu maalumu kwa ajili yao wawili tu.  Ni mchezo au mpango wa watu wawili, hivyo kuacha nje wengine wote.

Wakristo wote wenye shauku ya kuwa na nyumba bora ya kikristo lazima watambue kuwa katika macho ya ulimwengu thamani ya mtu inapimwa kwa, “thamani ya mali aliyo nayo? Lakini vitabu vya mbinguni vinaandika thamani yake kwa uwiano wa mema aliyo nayo? Lakini vitabu vya mbinguni vinaandika thamani yake kwa uwiano wa mema aliyoyakamilisha kwa kutumia mali alizokabidhiwa. [E.G. White 2 Selected Message Vol.2, 193]

Jambo la msingi katika “wawili kuwa mmoja”, ni kwamba watu wawili lazima wawe kamili wao wenyewe.  Watu wawili hawa wanahitaji kuwa watu wazima.  Ni kwa namna gani wanaweza kuwa watu wazima? Mtu anaweza kuwa mtu mzima kwa kuweza kuwajibika, kwa kutawala hisia, mwelekeo, tabia, uchaguzi, na mipaka yake.  Mtu aweza pia kuthibitisha kuwa mtu mzima kwa kutawala shauku, talanta na upendo wake.

Maadili Sita ya Msingi kwa Nyumba Bora ya Kikristo

Katika maisha ya leo tunatambua kuwa ipo haja kwa nyumba za Kikristo kuwa bora zaidi.  Ni kwa sababu wakati tunazo nyumba bora za Kikristo ni wazi tutakuwa wanafamilia bora na kama tuna wanafamilia bora kwa hakika tutakuwa na wakristo bora.  Kama tunao wakristo bora itakuwa wazi zaidi kuwa watu wengi watafaulu kuingia mbinguni.

Kwa hiyo yako maadili ambayo tunahitaji kuyajenga kama tunataka kuwa na nyumba bora za kikristo.  Tunahitaji kufikiri kwa upana na kuona picha kubwa ya maisha na nyumba zetu.  Hivyo kila mkristo anahitaji kujenga maadili yafuatayo:

1.       Utamaduni wa Upendo wa Yehova

Kama mtu ana shauku ya kupata juisi ya maembe ni wazi anahitaji kupanda miti ya maembe.  Kama anataka kupata juisi ya malimau lazima apande mti wa mlimao.  Hawezi kutegemea kupata juisi ya limao wakati anapanda miti ya miparachichi.  Haiwezekani kabisa!
Kwa utamaduni wa kumpenda Mungu ni maadili namba moja katika maisha ya mkristo.  Usitegemee kumpenda mtu yeyote kama humpendi Mungu.  Hata hivyo, ulimwengu unaweza kutuona kirahisi kama tuna upendo wa Mungu.  Kama ilivyothibitishwa katika Yohana 5:42 “lakini nawafahamu ninyi hamna upendo wa Mungu ndani yenu”.

Somo la kwanza:  kulingana na uzoefu wangu katika huduma ya ushauri nasaha tatizo kubwa ambalo familia inapata ni matokeo ya wanafamilia kusahau kumpa Mungu nafasi yake katika maisha yao na katika nyumba zao.

2.       Utamaduni wa upendo wa mwenzi wako

Mwenzi kwa ujumla amefasiliwa kuwa ni mbia wa mtu katika ndoa [Collins English Dictionary 2003].  Hivyo kabla hujajipenda mwenyewe unahitaji kwa kweli kumpenda mwenzi wako.  Hapa Biblia inatuambia kuwa tunahitaji kufuata mfano wa Yesu, ambaye ana utukufu wote mbinguni, lakini akaamua kushuka chini kwenye nafasi ya chini kuliko nafasi zote kama ilivyosemwa na Maxwell JN .  anaiita hii kuwa ni sheria ya kujitoa kwa hali ya juu.  [Fil 2:3-4] Kwa hiyo tunahitaji kufikiria mahitaji ya wenzi wetu kabla ya mahitaji yetu.

Katika maisha ya wanandoa upendo lazima uwe kitu namba moja katika yote watakayofanya iwe kwa siri au hadharani.  Wakati hili litakapoheshimiwa utukufu na heshima atapewa Bwana.

Somo la pili:  kwa ufahamu wangu familia yoyote inayohitaji kuwa na maisha bora, kila mwanafamilia lazima kwanza afikirie mambo yaw engine, au kuchukua mambo ya mwenzi wake kwanza.

3.       Utamaduni wa Ukweli/unyofu

Watu wengi katika jamii wamepoteza fikra ya unyofu.  Kamusi ya Collins, ya 2003, linafasili neon unyofu kama kuwa ni hali ya kuwa mkweli.  Unyofu unamaanisha kutokuwa na mwelekeo au tabia ya kudanganya, kusema uongo, kuiba au kutokuwa mkweli.

Familia nyingi ziko chini ya mvuto wa roho ya uovu na kama hii ndivyo ilivyo si rahisi kwa ukweli kuonyeshwa katika yote wanayopanga na kufanya.  Lakini pamoja na hayo Roho Mtakatifu kwa hakika ataijaza familia inayofundisha wanafamilia wake kuwa wakweli na hivyo kubadilisha maisha yao.  E.G. White anatushauri kuwa “hebu tabia yenu ifunue kiwango cha juu ambacho wote wanaweza kukifikia”.  [Ministry of Healing 198].

Anaendelea kutuambia kuwa katika ulimwengu huu waume na wanawake bado hawajaanza kuelewa makusudi ya kweli ya maisha.  Labda hii ni kwa sababu tumepoteza umaana wa unyofu katika maisha yetu na katika maisha ya familia.  Wakati tunaishi katika aina hiyo ya maisha, shetani anafurahi kwa sababu ni kusudi lake kutuona sisi hatuingii mbinguni ili kudhihirisha kuwa Mungu ni mbaya.

Sasa wale wote ambao tumekwisha kufahamishwa tunahitaji kwa kweli kuimarisha utamaduni wa kweli katika familia zetu.

Somo la tatu:  uzoefu wangu katika huduma ya ushauri nasaha ni kwamba matatizo mengi ambayo hayajatatuliwa katika familia yanasababishwa mara nyingi na wanafamilia ambao hawafuati sheria ya uaminifu – Kwa hiyo mwanafamilia yeyote ambaye anataka kuwa na familia bora ya kikristo anahitajika kuwa mwaminifu.  Uaminifu katika mambo makubwa na madogo.

4.       Utamaduni wa uaminifu

Je inamaanisha nini kuwa mwanimifu? Ni hali ya mtu ambaye ni mwaminifu.  Wakati mtu anapokuwa mwaminifu imesemwa kuwa, mtu Yule ana imani, anabaki kuwa mkweli, mwenye msimamo, na mtiifu.

Katika suala la maisha ya wenzi uaminifu utaamsha shauku ya maisha bora sio kwa mmoja bali kwa wote.

Katika maisha ya leo shetani anafurahi sana wakati mmoja wa wanandoa anapokuwa si mwaminifu.  Kwa sababu anafahamu kabisa kuwa hili litadhoofisha wanandoa na familia.  Hivyo wengi hawataingia mbinguni.  Uaminifu ni moja ya masharti ya maisha bora katika familia kwa wanandoa kuthaminiwa.  Ili kuwe na mafanikio katika maisha ya wanandoa, wabia hawa lazima wawe na umoja.  Hebu tuthaminiane kwa kuwa waaminifu.  Hivyo E.G. White anapendekeza kwetu kuwa “Thamani ya mwanaume au mwanamke kama Mungu anavyomkadiria ni katika muungano wake na Kristo [OHC 149]” Wakati tumeungana tunafanikiwa.

Somo la nne:  washauri wanaamini kuwa wanafamilia ambao wameamua au wamechagua kuishi maisha yasiyo ya uaminifu wanazalisha matatizo mengi katika familia.  Kwa hiyo mwanafamilia yeyote anaye tegemea maisha bora ya kifamilia anahitajika kuwa mwaminifu.

5.       Utamaduni wa huruma na msamaha

Utafiti wa neno huruma katika Biblia unaonesha kuwa neno huruma kwa kawaida linatumika kama sifa ya kiuungu na kibinadamu [New Bible Dictionary 1196].  Neno huruma linaweza kumaanisha hisia anazozipata mtu wakati ameguswa na mateso yaw engine, na tendo la kuingia ndani ya mateso yaw engine kwa makusudi ya kuyaondoa [New Dictionary of Christian Ethics and Pastoral Theology 2003].complete dictionary for home school and office chapisho la mwaka 1977 inafasili kuwa huruma ni kusikitishwa au kuwa na moyo wa huruma kwa mateso na mikasa ya wengine na kuwa na shauku ya kuwapa msaada au kuwaonyesha huruma.

Kwa upande mwingine, msamaha kwa ujumla unachukuliwa kuwa ni utambuzi kwamba toba ama ya mmoja au ya wote ni ya kweli na kwamba uhusiano mwema umerejeshwa au umepatikana [New Dictionary of Christian Ethics and Patoral Theology 2003].  

Msamaha ni vyote tendo la kusamehe na hali ya kusamehewa [  The Complete Dictionary for Home School and Office1977].
Maisha katika familia pasipo huruma na msamaha hayawezekani.  Nyumba bora ya kikristo inahitaji kujifunza roho ya huruma na msamaha.  Hii ndiyo thamani ambayo kila mmoja wetu kama mshiriki wa familia na wa nyumba lazima tusidhoofishe.  Nyumba nyingi za kikristo ziko mbali sana na kukamilisha hili.

Somo la tano:  kwa upande mmoja tunakuza tendo la kuwa na moyo wa huruma, na unaosamehe, na kwa upande mwingine tunakuza hali ya kusamehewa.  Yote mawili lazima yaende pamoja katika nyumba bora ya Kikristo.

6.       Utamaduni wa utakatifu

Kamusi ya New Dictionary of Christian Ethics and Pastoral Theology 1995, inafasili utakatifu kama kustahimili katika suala la ukweli na udanganyifu.  Wakati tunapoitazama Collins English Dictionary 2003 inaafiki kuwa utakatifu ni hali ya kuwa mtakatifu.
Kujifunza biblia kunaonesha kuwa utakatifu ni neno ambalo ni la kidini kabisa na ni sifa ya msingi ya Mungu.  [The New Dictionary of Christian Ethics and Pastoral Theology 1995].

Kila mwanafamilia lazima atambue kuwa tabia hii lazima ijengwe.  Ni katika hali hii Paul anasema kwamba, “Au hamjui ya kwamba miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu ambaye anakaa ndani yenu, mliyepewa na Mungu, na ninyi si mali yenu wenyewe?”

Ni kwa bahati mbaya kwamba washiriki wengi wa familia za kikristo wamechagua kuongoza chombo baharini kinyume na upande ule ambao Biblia inapendekeza katika maandishi ya Paulo.  Uchunguzi unaonesha kuwa matatizo mengi  katika familia yanatokea kwa sababu washiriki kwa makusudi kabisa wameamua kutozingati sifa hii ya Mungu.  Wanawaleta katika nyumba ya familia ya kikristo, marafiki, ndugu wa kiume wazazi na wengi wengine ambao hawataweza kuwasaidia kutafuta ufumbuzi wa hoja hizo bali watayafanya yawe mabaya zaidi.

Washiriki wote wa familia bora ya Kikristo lazima wajione wenyewe kuwa ni watakatifu na wametengwa kwa kila mmoja ajili ya mwenzake.

Hitimisho

Nyumba nyingi za kikristo hazina afya.  Hivyo haziwezi kuitwa nyumba bora za kikristo.  Kwa hiyo ipo haja ya kufanya matengenezo katika njia zetu za kuishi, kwa kuchagua mwenzi sahihi, kufunga milango ya nyumba zetu bora za kikristo, kuzifanya nyumba zetu za kikristo ziwe duara la ndani, kuwaacha wengine wote nje ya klabu, kwa sababu katika hali nyingi wa nje wanaathiri wa ndani.


This post first appeared on Afya Na Kiasi, please read the originial post: here

Share the post

IBADA: MAADILI SITA KWA NYUMBA YA KIKRISTO YENYE AFYA

×

Subscribe to Afya Na Kiasi

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×