Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

RONALDINHO APIGA 5,AGEUKIA UBALOZI PARALYMPIC

Mwana soka bora wa Dunia mwaka 2005 Ronaldo de Assis Moreira maarufu kama Ronaldinho alizua gumzo Hapo Jana baada ya kufunga magoli 5 kwenye michuano ya Indian Premier Futsa dhidi ya timu iliokuwa inaongozwa na Nguri wa Manchester United Paul Scholes.
Ronaldinho akishangilia hapo jana baada ya kufunga bao.
Ronaldinho ameamua kuikacha timu yake ya GOA ambayo aliiongoza vyema hapo jana kwa kushinda 7-2 dhidi ya timu ya BENGALURU na hatimaye mwanandinga huyo amegeukia mchongo mwingine.

Ronaldinho amepata dili la kuwa Balozi kwenye michuano ya Paralympic nchini Brazi.

Kabla ya ufafanuzi Paralympic ni nini? haya ni maneno ya Gaucho kuhusu Cafu ambaye ataenda kuziba pengo lake kwenye timu ya GOA.

"I am leaving you in great hands, Cafu, will replace me as your marquee player. He is a very dear friend and is a top quality player and I am sure he will light the league up."
Hata hivyo Gaucho amesema kuwa atarejea kwenye msimu wa pili wa Premier Futsal.

Cafu mwenye miaka 46 anaenda India ku-ungana na majina makubwa kama Ryan Giggs, Paul Scholes na Hernan Crespo nchini humo.

Paralympic ni Michezo mikubwa ya kimataifa inayohusisha watu wenye ulemavu mbalimbali mwilini.


This post first appeared on ELIYA95, please read the originial post: here

Share the post

RONALDINHO APIGA 5,AGEUKIA UBALOZI PARALYMPIC

×

Subscribe to Eliya95

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×