Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

IVO MAPUNDA ATAJIUNGA NA AFC LEOPARDS

Kipa mkongwe aliyekuwa akiichezea Azam FC, msimu uliopita Ivo Mapunda Atajiunga na klabu ya AFC Leopards ya inayoshiriki Ligi Kuu nchini Kenya baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja akiwa mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake wa miezi sita na Azam.
Mapunda
Mapunda  anajisikia furaha kurudi kwenye ligi ya Kenya, kwasababu ndiyo ligi iliyomfanya ajulikane kwenye taifa hilo wakati alipokuwa akiichezea Gor Mahia na kuipa ubingwa wa kwanza baada ya muongo mmoja mwaka 2013.
“Hii ni nafasi pekee kwangu kuonyesha kipaji kuwa bado ninauwezo nitahakikisha naisaidia Leopard kwasababu nakwenda kama kipa ambaye najulikana kutokana uwezo wangu baada ya timu za nyumbani kuniona mzee nimepitwa na wakati,”amesema Mapunda.
Kwa kutua kwake Leopards Mapunda atakuwa ni mchezaji wa kwanza aliyewahi kuzichezea timu kubwa zenye upinzani katika nchi mbili tofauti za Afrika Mashariki na Kati kwa nyumbani Tanzania alianza kuichezea Yanga na baadaye alisajiliwa na Yanga na sasa ametua Leopards baada ya kuichezea kwa mafanikio Gor Mahia timu ambazo zinaupinzani mkali kwenye ligi ya Kenya.


This post first appeared on ELIYA95, please read the originial post: here

Share the post

IVO MAPUNDA ATAJIUNGA NA AFC LEOPARDS

×

Subscribe to Eliya95

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×