Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Makonda Azindua Hospitali ya Mama na Mtoto Iliyojengwa kwa Jitihada Zake




Rais wa Shirika la Misaada la Korea Kusini Koica Bi.Lee Mi Kyung amezindua hospitali ya Mama na Mtoto Chanika iliyojengwa kwa jitiada binafsi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda alietafuta wafadhili hao.

Ujenzi wa hospitali hiyo ya kisasa umegarimu zaidi shillingi billion 9.8 ambapo ndani kuna vyumba vya kisasa vya upasuaji, vyumba vya madaktari, maabara,chumba cha mionzi, wodi ya wazazi,wodi ya watoto njiti, Theater, vyumba vya kujifungulia, ICU, Vyoo vya kisasa pamoja na nyumba za Familia 28 za madaktari ambapo ndani ya nyumba hizo kuna kila kitu.



RC Makonda amesema aliamua kutafuta wafadhili wa kujenga hospitali hiyo baada ya kuona kilio cha kinamama waliokuwa wakipoteza maisha na watoto baada ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma za Afya.

Aidha RC Makonda amemuomba Rais wa KOICA kumjengea Hospital nyingine mbili kwenye Wilaya mpya za Ubungo na Kigamboni ili kusaidia maboresho ya huduma za afya.

Pamoja na hayo RC Makonda ameshukuru serikali ya Korea kusini kwa ufadhili wa hospital hiyo yenye hadhi ya kimataifa.

kwa upande wake Rais wa KOICA Bi. Lee Mi Kyung amesema shirika hilo litaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania katika masuala mbalimbali ya maendeleo huku akipongeza Tanzania kwa kudumisha amani tofauti na Mataifa mengine.

Uzinduzi wa Hospital hiyo umeenda sambamba na uzinduzi wa magari mawili ya kisasa ya wagonjwa (ambulance).

Bongo5.com




This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Makonda Azindua Hospitali ya Mama na Mtoto Iliyojengwa kwa Jitihada Zake

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×