Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Makonda Awatolea Uvivu Wanaomsema Vibaya


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema wale wote wanaosema kampeni yake ya kuwasaidia akina mama waliotelekezwa na Watoto imevunja sheria, pengine wana watoto nje na wanaogopa kujitokeza.

Makonda ameyasema hayo leo Aprili 19,2018 katika uzinduzi wa hospitali ya kisasa ya mama na mtoto iliyopo Chanika iliyojengwa kwa msaada wa Shirika Maendeleo la Kimataida la Korea (Koica).

“Eti wanasema navunja sheria, natakiwa nifanye faragha kama unataka faragha tunza mtoto. Mimi siogopi, nipo tayari kufungwa lakini kwa ajili wa kutetea haki za watoto. Pengine hao wanaosema navunja sheria wana watoto wao nje wanaogopa kujitokeza,” amesema.

Jana, Waziri wa Sheria na Katiba, Profesa Palamagamba Kabudi akiwa bungeni Alisema Kampeni Hiyo inaweza kuleta hali ya sintofahamu na akabainisha kuwa inapaswa kufanyika faragha na sio kama inavyofanyika sasa.

Awali, Waziri wa Afya, Jinsia, Wanawake na Watoto, Ummy Mwalimu alisema kampeni hiyo ni sahihi ila kasoro yake ni kutokuwa na faragha, lakini akasema kwa sasa inafanyika huku picha za watoto zikifichwa.

Aliyeibua hilo bungeni jana alikuwa ni mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga aliyehoji uhalali wa kampeni hiyo na akahoji kama haivunji sheria na kuwavunjia haki wanawake na watoto.


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Makonda Awatolea Uvivu Wanaomsema Vibaya

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×