Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Utetezi wa Naibu Spika Kwa Mawaziri



Naibu Spika, Tulia Ackson amewatetea mawaziri ambao wanashutumiwa kwa kutumia Vyombo Vya Habari kujibu hoja za ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali wiki iliyopita.

Tangu Alhamisi ya wiki iliyopita, mawaziri wanne akiwamo wa Habari, Utamaduni na Michezo; waziri wa Fedha na Mipango na waziri wa Viwanda na Biashara walijumuika na kufanya mkutano na wanahabari wakijibu hoja za ripoti ya CAG.

Kitendo cha mawaziri hao kilikosolewa na wengi akiwamo Mbunge wa Kigoma Mjini, (ACT-Wazalendo) Zitto Kabwe.

Akizungumza bungeni leo Aprili 16, Dk Ackson amesema mawaziri hao walikuwa wakitoa maoni yao kwa vyombo vya habari na si kujibu ripoti ya CAG.

“Kama ambavyo sheria isivyozuia CAG kuzungumza na vyombo vya habari, hivyo hivyo sheria haiwazuii mawaziri kutoa maoni yao kwa vyombo vya habari kuhusu ripoti ya CAG,” amesema Dk Ackson.

Hata hivyo amesema ni wajibu wa maofisa masuhuli kujibu ripoti ya CAG na kuwa hayo yanatakiwa kufanywa na mchakato wa Bunge.

MPEKUZI


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Utetezi wa Naibu Spika Kwa Mawaziri

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×