Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Watu Watano Wamefariki Dunia Wilayani Moshi Baada ya Kung’atwa na Mbwa Wenye Kichaa.


Watu watano wamefariki Dunia Wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro baada ya kung’atwa na mbwa wenye kichaa.
Daktari bingwa wa magonjwa ya dharura na ajali wa Hospitali ya Rufaa ya KCMC, Dk Francis Sakita amewaambia wanahabari leo Aprili 12,2018 kuwa ugonjwa huo umekuja kwa kasi kubwa ukilinganisha na miaka mingine.
Amesema kwa kipindi cha Januari hadi Machi vimetokea vifo vitano.

"Hii sio hali ya kawaida kutokea idadi kubwa ya watu kufariki dunia kwa kung'atwa na mbwa wenye ugonjwa huu, idadi hii ni kubwa sana na wengi walioathirika ni watu ambao wako Moshi vijijini. Hii inatokana na watu kutozingatia kupeleka mbwa wao kwenye chanjo," amesema Dk Sakita.
Malunde.com


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Watu Watano Wamefariki Dunia Wilayani Moshi Baada ya Kung’atwa na Mbwa Wenye Kichaa.

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×