Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Lwandamina aiweka Yanga kizani



KOCHA Mzambia, George Lwandamina ameondoka Kwenda Zambia na habari zinasema anarejea Zesco United ya kwao.

Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa alisema kuwa Lwandamina hajatokea mazoezini juzi asubuhi bila sababu na wanamtafuta hapatikani.

“Mimi sijui kaenda wapi, kwa sababu hajaniaga,hizo habari (za kwenda Zambia) wewe ndiyo unaniambia,”alisema Mkwasa.

Habari zinasema kwamba Zesco United imeamua kumrejesha kocha wake huyo baada ya mafanikio yake Tanzania ndani ya miaka miwili, akiiwezesha kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu uliopita na sasa inakaribia kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Yanga SC imejiweka kwenye nafasi nzuri ya kwenda hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho la Afrika baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Wolaita Ditcha ya Ethiopia katika mchezo wa kwanza wa mchujo wa kuwania kuingia hatua hiyo Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ushindi huo uliotokana na mabao ya Raphael Daudi kipindi cha kwanza na Emmanuel Martin kipindi cha pili, unamaanisha Yanga SC watahitaji kwenda kulazimisha sare ugenini wiki ijayo, au kutofungwa zaidi ya tofauti ya bao moja ili kwenda hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho kwa mara ya pili baada ya mwaka 2016.

Na Lwandamina ambaye mkataba wake unamalizika Juni mwaka huu, anaondoka Yanga siku moja kabla ya kuteremka uwanjani kumenyana na Singida United katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo walitoka Suluhu ya 1-1

Zanzibarleo


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Lwandamina aiweka Yanga kizani

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×