Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Roma Yafanya Maajabu, Yatinga Nusu Fainal, Man City Nayo Yakwama Etihad Stadium



Roma imefanya maajabu baada ya kuwabamiza Barcelona 3-0 na hivyo kutinga nusu fainali za mabingwa Ulaya kwa faida ya goli la ugenini.

Barca walikuwa wanapewa nafasi kubwa ya kusonga mbele kutokana na kuingia uwanjani wakiwa na akiba ya magoli, ambapo kutokana na mechi ya kwanza waliyoipiga Roma bao 4-1, Roma ilikuwa inalazimika kuifunga Barcelona 3-0.

Goli la Edin Dzeko dakika za awali za mchezo (6'), na Penalty ya Daniele de Rossi katika kipindi cha pili dakika ya 58 yamekamilishwa na Goli la Mlinzi Kostas Manolas alilofunga zikiwa zimesalia dakika nane tu mechi kufikia mwisho zimewafanya Barcelona pamoja nakuwa na Lionell Messi ambaye hakufurukuta, kuondokakichwa chini katika Ligi ya mabingwa barani Ulaya.

Umati uliokuwepo Stadio Olimpico ulilipuka mara baada ya kipyenga cha mwisho pale wachezaji wa akiba wa Roma na benchi lao la ufundi walipoingia katikati ya uwanja kushangilia na wachezaji wao.

Kulikuwa na machozi katika nyuso za mashabiki wasiamini kile walichokishuhudia katika mtanange huo ambao haukutegemewa kuisha ulivyoisha.



Roma imekuwa timu ya tatu katika Champions League kuweza kuyapindua matokeo ya namna hiyo ya goli tatu au zaidi. Timu pekee mbili ambazo awali ziliwahi kufanya hivyo ni Deportivo La Coruna dhidi ya AC Milan mwaka 2004 na Barcelona dhidi ya Paris St-Germain msimu uliopita.


Liverpool imefika katika nusu fainali yao ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa kwa miaka 10 baada ya kujikokota na kuishinda Manchester City kwa kupata ushindi wa mabao 2-1 yaliyoleta ushindi wa jumla wa Liverpool 5-1 Man City.

City walianza vizuri wakati walipojaribu kulipa deni la 3-0 walizofungwa katika mechi ya kwanza. Ilikuwa dakika ya pili tu ya mchezo ambapo Raheem Sterling alimwanzishia Gabriel Jesus aliyeitumia nafasi hiyo kupachika bao la kuwapa matumaini Man City. Hata hivyo baada ya tukio la vurugu kabla ya muda wa mapumziko lililoisha kwa Meneja Pep Guardiola kuondoshwa katika eneo la benchi la ufundi, City hawakuweza kuyafikia matamanio yao.

Tukio lenyewe lilianzia pale ambapo Bernardo Silva alikuwa amepiga mkwaju kuelekea lango la Liverpool, huku Liverpool ikiwa katika shinikizo zito, mpira ukamkuta Leroy Sane ambaye aliukwamisha wavuni na kuwafanya City kudhani wamefanikiwa kupata goli la pili.

Lakini hali ilikuwa tofauti kwani mwamuzi Antonio Mateu Lahoz alilikataa goli hilo kwa madai kuwa limepatikana katika mazingira ya kuotea yaani offside, jambo ambalo limemkera Pep Guadiola aliyeingia uwanjani kumkabili mwamuzi Antonio Mateu Lahoz, na hivyo meneja huyo wa City kuambulia kufukuzwa katika eneo lake la ufundi hali iliyomfanya kulazimika kuitizama kipindi cha pli akiwa katika viti vya mashabiki.

City wakijaribu kupambana katika mazingira ambayo mwalimu wao yuko mbali, wakapoteza mwamko na kuwapa nafasi wageni Liverpool kupitia Mohamed Salah akajipatia bao lake la 39 la msimu baada ya mbio za nguvu kutoka kwa Sadio Mane mnamo dakika ya 56.

Goli zuri la Robert Firmino dakika 13 kabla ya kumalizika kwa mchezo, limekuwa msumali wa mwisho katika jeneza la Man City na hivyo kuwahakikishia Liverpool kusonga mbele.

Sasa Liverpool wanasubiri kuwajua wapinzani wao katika nusu fainali wakati droo itakapochezeshwa Ijumaa [12:00 BST] huko Nyon, Uswisi.

BBC Swahili


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Roma Yafanya Maajabu, Yatinga Nusu Fainal, Man City Nayo Yakwama Etihad Stadium

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×