Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Simba Yaendeleza Kipigo

Simba SC imeendelea kujikusanyia Alama katika Ligi Kuu Bara baada ya kuilaza Mtibwa Sugar FC kwa bao 1-0 jioni ya jana Kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Mchezo huo uliokuwa unaambatana na mvua iliyokuwa ikinyesha Uwanjani, ulishuhudiwa nyavu zikitikiswa mnamo dakika ya 24 ya kipindi cha kwanza na Emmanuel Okwi.

Okwi alifunga bao hilo akimalizia kazi mpira wa kichwa kutoka kwa John Bocco na kufanya mchezo huo udumu kwa dakika zote 90 huku matokeo yakisalia kuwa 1-0.

Matokeo hayo yanaifanya Simba izidi kujikita kileleni kwa kufikisha alama 52 dhidi ya watani wao wa jadi Yanga wenye 46 mpaka sasa.

Mechi inayofuatia kwa Simba itakuwa dhidi ya Wajelajela Mbeya City FC, itakayopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Simba Yaendeleza Kipigo

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×