Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Maandamano ya Michezo Yapangwa Siku ya Tarehe 26 April



Halmashauri ya jiji la Arusha imeaanda maandamano makubwa ya michezo ambayo yatafanyika siku ya sherehe ya maadhimisho muungano April 26, 2018 jijini Arusha

Afisa michezo wa jiji la Arusha, Benson Maneno amethibitisha hilo na kusema kuwa maandamano hayo yatafanyika asubuhi kuelekea katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Karume ambapo ndipo zitafanyika fainali za michuano ya Muungano Cup na kumpata mshindi wa michuano hiyo, ambapo mshindi wa kwanza atapata milioni mbili, mshindi wa pili milioni moja na mshindi wa tatu laki tano.

"Mashindano hayo ambayo yameanzishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa jiji la Arusha akishilikiana na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Dakalo wameanzisha mashindano haya maalum kwa kata zote 25 ambapo watashirikisha vijana wenye umri chini ya miaka 26, hivyo kila kata itacheza na kata nyingine ili kupata mshindi wa michuano hiyo.

"Fainali hizo zitafanyika jioni lakini asubuhi ya tarehe 26 kutakuwa na maandamano makubwa ya wana michezo kuelekea uwanja wa Sheikh Amri Abeid Karume kwa ajili ya kufanya fainali hiyo ya Muungano CUP" alisema Benson Maneno

Lakini kwa upande mwingine, siku hiyo hiyo ya Muungano 26 April, 2018 watu mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii wakiongozwa na mwanaharakati wa mitandao Mange Kimambi pia wamepanga kufanya maandamano ya nchi nzima kupinga baadhi ya vitu ambavyo vinaendelea nchini kwa sasa.


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Maandamano ya Michezo Yapangwa Siku ya Tarehe 26 April

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×