Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Magufuli Kupokea Magari 181 ya Kusambazia Dawa Nchini


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Machi 26, 2018 anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika Kupokea Magari 181 ambayo yatakuwa yakitumika kusambaza madawa vijijini na mjini.

Taarifa hiyo iliyotolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas imeweka wazi kuwa Rais Magufuli ndiye atakuwa mgeni rasmi na kuzindua magari hayo 181 yaliyopo chini ya Bohari Kuu ya Dawa (MSD).

"Mageuzi Sekta ya Afya yanaendelea, usikose hafla ya kupokea magari mapya 181 kufikisha dawa na vifaa tiba zaidi mijini na vijijini" alisema Dkt Abass


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Magufuli Kupokea Magari 181 ya Kusambazia Dawa Nchini

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×