Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Mei Mosi 2018 Kitaifa Kufanyika Jijini Arusha


Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (Tuico), kimeanza maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei mosi), yanayotarajiwa kufanyika kitaifa mkoani Arusha.

Mwenyekiti wa Tuico taifa, Paulo Sangeze, alisema, mgeni rasmi katika maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Rais John Magufuli.

Akizungumza katika semina ya kuelimisha na kubadilishana uzoefu, iliyowashirikisha viongozi wa matawi mbalimbali ya Tuico mwishoni mwa wiki, iliyofanyika jijini hapa, Mwenyekiti wa Tuico taifa, Sangeze, alisema Shirikisho la Vyama vya Huru vya Wafanyakazi nchini (Tucta), limekiteua chama chao kuwa mratibu wa shughuli zote za Mei mosi kwa mwaka huu.

Alisema baada ya kupewa fursa hiyo wanafanya vikao vya maandalizi na tayari wamepanga maadhimisho hayo kwa mwaka huu, yatafanyika mkoani Arusha katika Uwanja wa mpira wa Sheikh Amri Abeid.

Katibu wa Tuico, Boniface Nkakatisi, alisema maandalizi hayo yanaenda na mialiko ya wageni watakaohudhuria ikiwamo wafanyakazi mbalimbali nchini, wanachama wa Tuico, mabalozi kutoka nchi mbalimbali duniani.


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Mei Mosi 2018 Kitaifa Kufanyika Jijini Arusha

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×