Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Tetesi za soka Ulaya Jumamosi Ya Tarehe 17 Machi 2018


Real Madrid imekubali kusajili Mshambuliaji wa Bayern Munich na timu ya taifa ya Poland Robert Lewandowski.

Mshambuliaji huyo mwenye miaka 29 pia anafuatiliwa na klabu za Chelsea na Manchester United.(Mundo Deportivo )

Mlinzi wa kati wa Real Madrid Raphael Varane amesema Manchester United inamuhitaji. Mfaransa huyo mwenye miaka 24 alisajiliwa klabuni hapo chini ya Jose Mourinho.(Cadena Ser, via Sun)

Kiungo wa zamani wa Liverpool na Bayern Munich Dietmar Hamann amesema Bayer wanazungumza na kocha wa Tottenham Mauricio Pochettino juu ya uwezekano wa kuwanoa.(Sky, via Mirror)

Everton iko tayari kumlipa kiungo wa Arsenal Jack Wilshere ambaye mkataba wake na Gunners unaisha mwisho wa msimu huu.Wapo tiyari kumpa paundi milioni 8 kwa mwaka iwapo atasajiliwa bure.(Times )

Borussia Dortmund wameonyesha nia ya kumsajili kiungo mshambuliaji wa Westham mreno Domingos Quina.(Sun)

Spurs wanatarajia kufanya mazungumzo ya kumpa mkataba mpya mshambuliaji raia wa Korea Kusini Son Heung-min.Mkataba wake wa sasa unaishia mwaka 2020.(Sky Sports)

Meneja msaidizi wa Leicester city Michael Appleton yupo miongoni mwa makocha wanaowaniwa na West Brom kuziba nafasi ya Alan Pardew.(Telegraph)

Mlinda mlango wa Roma Alisson anahusishwa kujiunga na Liverpool lakini matamanio yake ni kwenda Real Madrid.(Express)

Meneja wa Chelsea Antonio Conte amesema mlinzi wa kati Gary Cahill na mshambuliaji Alvaro Morata wanahitaji juhudi zaidi iwapo wanataka kurejea katika kikosi cha kwanza na kuweka uwezekano wa kuziwakilisha timu zao za taifa ambazo ni Uingereza na Hispania.(Express)

Conte anaamini hawezi ondolewa kwenye klabu ya Chelsea iwapo mabingwa hao wa msimu uliopita hawatafuzu kucheza klabu bingwa ulaya msimu ujao.(Telegraph)


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

Tetesi za soka Ulaya Jumamosi Ya Tarehe 17 Machi 2018

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×