Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUAHIRISHWA KWA USAILI WA 08-09 JUNI 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Tanzania Metrological Agency (TMA), Tanzania Meat Board (TMB), The Local Government Training Institute (LGTI) na Registration, Insolvency And Trusteeship Agency (RITA) alitoa tangazo katika tovuti ya Sekretarieti ya Ajira la kuita kwenye usaili tarehe 1 Juni, 2016 waombaji wa kazi waliowasilisha maombi na kukidhi vigezo kwa taasisi zilizoanishwa hapo juu. Kupitia tangazo hili Waombaji kazi wote waliotangaziwa kuitwa kwenye usaili kwa tangazo hilo wanafahamishwa kuwa usaili huo umeahirishwa mpaka hapo watakapotangaziwa tena hapo baadaye. Kwa Matangazo ya nafasi za kazi yaliyotolewa mnamo tarehe 6 Mei, 2016, 11 Mei, 2016, 18 Mei, 2016 na tarehe 26 Mei, 2016 nayo waombaji kazi watakaokidhi vigezo watataarifiwa hapo baadae kuhusu mchakato wake unavyoendelea. Aidha, Kupitia tangazo hili, Sekretarieti ya Ajira kwa niaba ya Serikali inaomba radhi waombaji kazi wote waliowasilisha maombi na wale waliokuwa wamejiandaa kuhudhuria usaili huo kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUAHIRISHWA KWA USAILI WA 08-09 JUNI 2016

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×