Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

UJENZI WA BANDARI YA LAGOSA WAFIKIA 90%


Serikali ipo katika hatua za mwisho kukamilisha Ujenzi wa Bandari ya Lagosa iliyopo katika Kijiji cha Mgambo wilayani Uvinza mkoani Kigoma.

Akizungumza mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo Waziri wa Uchukuzi Prof.Makame Mbarawa amesema ujenzi huo unaogharimu shilingi bilioni kumi na Tano tayari umefikia asilimia tisini na sita na kusisitiza ifikapo mwezi Aprili mwaka 2024 mradi huo uwe umekamilika .

Aidha Prof.Mbarawa amesema uwepo wa Bandari Hiyo utachagiza ufanisi wa shughuli za kiuchumi hasa kilimo ,uvuvi na biashara kwa wakazi wa mwambao wa ziwa Tanganyika ambao kupitia bandari hiyo wataweza kusafiri na kusafirisha bidhaa zao kwenda nje ya nchi.

Kwa upande wake naibu mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya usimamizi wa bandari Tanzania TPA mhandisi Juma Kijavara amesema TPA imejipanga kukamilisha ujenzi huo haraka ili bandari hiyo ianze kutoa huduma kwa wananchi.

Naye mkuu wa wilaya ya uvinza Dina Masamani ameishukuru serikali kwa kujenga bandari hiyo akisisitiza kuwa itawezesha wakazi kufanya shughuli za kiuchumi na kijamii ikiwemo kusafirisha bidhaa kwenda nchi Jirani ya Congo ambayo ipo umbali wa Kilometa themanini na nane kutoka bandarini hapo.



This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

UJENZI WA BANDARI YA LAGOSA WAFIKIA 90%

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×